2 Mambo ya Nyakati 34:1-33

34  Yosia+ alikuwa na umri wa miaka 8+ alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 31 katika Yerusalemu.+  Naye akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova+ na kutembea katika njia za Daudi babu yake;+ naye hakugeuka kando upande wa kuume wala wa kushoto.+  Na katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, alipokuwa angali mvulana,+ akaanza kumtafuta+ Mungu wa Daudi babu yake; na katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kutakasa+ Yuda na Yerusalemu kutokana na mahali pa juu+ na miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ na sanamu za kuyeyushwa.  Tena wakabomoa mbele yake zile madhabahu+ za Mabaali;+ na vile vinara vya uvumba+ vilivyokuwa juu akavikata kutoka juu yazo; na ile miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ na sanamu za kuyeyushwa akazivunja vipande-vipande na kuzifanya kuwa mavumbi,+ kisha akayanyunyiza juu ya uso wa makaburi ya wale waliokuwa wakizitolea dhabihu.+  Na mifupa+ ya makuhani akaiteketeza juu ya madhabahu zao.+ Kwa hiyo akatakasa Yuda na Yerusalemu.  Pia, katika majiji ya Manase+ na Efraimu+ na Simeoni na mpaka Naftali, katika mahali pao palipoharibiwa kuzunguka pande zote,  hata alibomoa madhabahu+ na miti mitakatifu,+ na sanamu za kuchongwa+ akaziponda na kuzifanya kuwa mavumbi;+ na vinara vyote vya uvumba+ akavikata katika nchi yote ya Israeli, kisha akarudi Yerusalemu.  Na katika mwaka wa kumi na nane+ wa kutawala kwake, alipokuwa ameitakasa nchi na nyumba, akawatuma Shafani+ mwana wa Azalia na Maaseya mkuu wa jiji na Yoa mwana wa Yoahazi karani wakarekebisha+ nyumba ya Yehova Mungu wake.  Nao wakamjia Hilkia+ kuhani mkuu na kumpa pesa zilizokuwa zikiletwa katika nyumba ya Mungu, ambazo Walawi watunza-milango+ walikuwa wamekusanya kutoka mkononi mwa Manase+ na Efraimu+ na kutoka kwa wale wengine wa Israeli+ na kutoka kwa Yuda wote na Benyamini na wakaaji wa Yerusalemu. 10  Kisha wakazitia mkononi mwa wafanyakazi waliowekwa juu ya nyumba ya Yehova.+ Nao wafanyakazi waliokuwa wakitenda kazi katika nyumba ya Yehova wakazitumia kutengeneza na kuirekebisha nyumba. 11  Basi wakawapa mafundi na wajenzi+ ili wanunue mawe yaliyochongwa+ na mbao kwa ajili ya vibanio na kujenga kwa boriti zile nyumba ambazo wafalme+ wa Yuda walibomoa. 12  Na watu hao walikuwa wakifanya kazi ile kwa uaminifu;+ na juu yao wakawekwa Yahathi na Obadia, Walawi, kutoka kwa wana wa Merari,+ na Zekaria na Meshulamu, kutoka kwa wana wa Wakohathi,+ wawe waangalizi. Na Walawi, ambao kila mmoja wao alikuwa mjuzi wa vyombo vya nyimbo,+ 13  walikuwa juu ya wabeba-mizigo,+ na waangalizi+ wa wafanyakazi wote kwa ajili ya utumishi mbalimbali; na kutoka kwa Walawi+ kulikuwa na waandishi+ na maofisa na watunza-malango.+ 14  Sasa walipokuwa wakitoa pesa+ zilizokuwa zinaletwa katika nyumba ya Yehova, Hilkia+ kuhani akakipata kile kitabu+ cha sheria ya Yehova+ kupitia mkono wa Musa.+ 15  Kwa hiyo Hilkia akamjibu na kumwambia Shafani+ mwandishi: “Nimepata kile kitabu chenyewe cha sheria katika nyumba ya Yehova.” Basi Hilkia akampa Shafani kile kitabu. 16  Kisha Shafani akampelekea mfalme kile kitabu, akaendelea kumjibu mfalme, akisema: “Yote ambayo yametiwa mkononi mwa watumishi wako wanayafanya. 17  Nao wanamimina pesa ambazo zimo ndani ya nyumba ya Yehova na kuzitia katika mkono wa watu waliowekwa na katika mkono wa wale wanaofanya kazi.”+ 18  Na Shafani mwandishi akaendelea kumletea mfalme habari, akisema: “Hilkia kuhani amenipa+ kitabu+ fulani.” Na Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.+ 19  Na ikawa kwamba mara tu mfalme alipoyasikia maneno ya ile sheria, akayararua mavazi yake mara moja.+ 20  Kisha mfalme akawaamuru Hilkia+ na Ahikamu+ mwana wa Shafani na Abdoni mwana wa Mika na Shafani+ mwandishi+ na Asaya+ mtumishi wa mfalme, akisema: 21  “Nendeni, muulizeni+ Yehova kwa ajili yangu+ na kwa ajili ya mabaki katika Israeli na katika Yuda kuhusu maneno ya kile kitabu+ ambacho kimepatikana, kwa maana ghadhabu ya Yehova ambayo itamwagwa juu yetu ni kubwa+ kwa sababu mababu zetu hawakulishika neno la Yehova kwa kutenda kulingana na yote ambayo yameandikwa katika kitabu hiki.”+ 22  Basi Hilkia pamoja na wale ambao mfalme alikuwa amesema wakaenda kwa Hulda+ nabii,+ mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi mtunzaji wa mavazi,+ kwa kuwa alikuwa akikaa Yerusalemu katika eneo la pili; nao wakaanza kusema naye hivyo. 23  Naye akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Mwambieni hivi mtu ambaye amewatuma ninyi kwangu: 24  “Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba+ juu ya mahali hapa na wakaaji wake,+ laana+ zote ambazo zimeandikwa katika kile kitabu walichosoma mbele ya mfalme wa Yuda,+ 25  kwa sababu wameniacha+ na kwenda kuifukizia moshi wa dhabihu miungu mingine,+ ili kunitia uchungu+ kwa matendo yote ya mikono yao,+ na ili ghadhabu+ yangu imwagike juu ya mahali hapa wala isizimwe.’”+ 26  Na mfalme wa Yuda, anayewatuma mkamuulize Yehova, mwambieni hivi: “Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi,+ ‘Kuhusu yale maneno+ ambayo umeyasikia, 27  kwa sababu moyo+ wako ulikuwa mwororo hivi kwamba ukajinyenyekeza+ kwa sababu ya Mungu uliposikia maneno yake kuhusu mahali hapa na wakaaji wake, nawe ukajinyenyekeza mbele zangu,+ ukayararua+ mavazi yako na kulia mbele zangu, mimi, naam, mimi nimesikia,+ asema Yehova. 28  Tazama, nitakukusanya wewe kwa mababu zako, nawe hakika utakusanywa kwenye uwanja wa kaburi lako kwa amani,+ na macho yako hayatauona msiba+ wote ninaouleta juu ya mahali hapa na wakaaji wake.’”’”+ Ndipo wakamletea mfalme jibu. 29  Na mfalme akatuma na kukusanya wanaume wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.+ 30  Sasa mfalme akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova+ akiwa na wanaume wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu na makuhani+ na Walawi na watu wote, wakubwa kwa wadogo; naye akaanza kusoma+ masikioni mwao maneno yote ya kile kitabu cha agano, kilichokuwa kimepatikana katika nyumba ya Yehova.+ 31  Na mfalme akaendelea kusimama mahali pake+ naye akafanya agano+ mbele za Yehova ili kumfuata Yehova na kushika amri+ zake na shuhuda+ zake na masharti+ yake kwa moyo wake wote+ na kwa nafsi yake yote,+ ili kutenda+ yale maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.+ 32  Na zaidi ya hayo, akawafanya wale wote waliopatikana katika Yerusalemu na Benyamini wachukue msimamo wao katika hilo. Na wakaaji wa Yerusalemu wakafanya kulingana na agano la Mungu, Mungu wa mababu zao.+ 33  Kisha Yosia akaondoa machukizo+ yote kutoka katika nchi zote za wana wa Israeli,+ naye akawafanya wote waliopatikana katika Israeli wachukue utumishi, wamtumikie Yehova Mungu wao. Siku zake zote hawakugeuka kando wasimfuate Yehova Mungu wa mababu zao.+

Maelezo ya Chini