2 Mambo ya Nyakati 33:1-25

33  Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 55 katika Yerusalemu.+  Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na machukizo+ ya mataifa ambayo Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+  Kwa hiyo akajenga tena mahali pa juu+ ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akasimamisha madhabahu+ kwa Mabaali+ na kutengeneza miti mitakatifu,+ naye akaanza kuliinamia+ jeshi lote la mbinguni+ na kulitumikia.+  Naye akajenga madhabahu+ katika nyumba ya Yehova, ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Jina langu litakuwa katika Yerusalemu mpaka wakati usio na kipimo.”+  Naye akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili+ za nyumba ya Yehova.+  Naye mwenyewe akawapitisha wanawe mwenyewe motoni+ katika bonde la mwana wa Hinomu,+ akafanya uchawi+ na kutumia uaguzi+ na kufanya ulozi+ na kufanyiza wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio. Alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, na kumtia uchungu.+  Zaidi ya hayo, akaweka sanamu ya kuchongwa+ aliyokuwa ametengeneza katika nyumba ya Mungu wa kweli,+ ambayo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na Sulemani mwana wake hivi kuihusu: “Katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambalo nimelichagua+ kutoka katika makabila yote ya Israeli, nitaliweka jina langu+ mpaka wakati usio na kipimo.+  Nami sitauondoa mguu wa Israeli tena utoke katika nchi niliyowagawia+ mababu zao,+ mradi tu wawe waangalifu kufanya yote ambayo nimewaamuru+ kuhusiana na sheria+ yote na masharti+ na maamuzi ya hukumu+ kupitia mkono wa Musa.”+  Na Manase+ akaendelea kuwashawishi Yuda+ na wakaaji wa Yerusalemu wafanye mabaya zaidi+ kuliko yale mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+ 10  Na Yehova akaendelea kusema na Manase na watu wake, lakini hawakusikiliza.+ 11  Mwishowe Yehova akaleta juu yao+ wakuu wa jeshi la mfalme wa Ashuru,+ nao wakamteka Manase katika mashimo+ na kumfunga+ kwa pingu mbili za shaba, wakampeleka Babiloni. 12  Na mara tu jambo hilo lilipomtaabisha,+ akautuliza uso wa Yehova Mungu wake,+ akaendelea kujinyenyekeza+ sana kwa sababu ya Mungu wa mababu zake. 13  Naye akaendelea kusali kwake Yeye, hivi kwamba Yeye akakubali kusihiwa+ naye kisha Yeye akasikia ombi lake la kutaka kibali, akamrudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake;+ na Manase akapata kujua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+ 14  Na baada ya hayo akajenga ukuta wa nje+ kwa ajili ya Jiji la Daudi+ upande wa magharibi wa Gihoni+ katika bonde la mto na mpaka Lango la Samaki,+ akauzungusha mpaka Ofeli+ na kuufanya kuwa mrefu sana. Tena akaweka wakuu wa jeshi katika majiji yote yenye ngome katika Yuda.+ 15  Naye akaiondoa miungu ya kigeni+ na ule mfano wa sanamu+ kutoka katika nyumba ya Yehova na madhabahu+ zote alizokuwa amejenga katika mlima wa nyumba ya Yehova na katika Yerusalemu, kisha akavitupa nje ya jiji. 16  Tena akatayarisha madhabahu ya Yehova+ na kuanza kutoa juu yake dhabihu za ushirika+ na dhabihu za shukrani,+ akaendelea kuwaambia Yuda wamtumikie Yehova Mungu wa Israeli.+ 17  Hata hivyo, watu walikuwa bado wanatoa dhabihu katika mahali pa juu;+ ila tu ilikuwa ni kwa Yehova Mungu wao. 18  Na yale mambo mengine ya Manase na sala+ yake kwa Mungu wake na maneno ya waonaji+ walioendelea kusema naye katika jina la Yehova Mungu wa Israeli, tazama, yamo kati ya mambo ya wafalme wa Israeli.+ 19  Na kuhusu sala+ yake na jinsi ombi+ lake lilivyojibiwa na dhambi+ yake yote na ukosefu wake wa uaminifu+ na vile vituo, mahali ambapo alijenga mahali pa juu+ na kusimamisha miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ kabla ya kujinyenyekeza,+ tazama, yameandikwa kati ya maneno ya waonaji wake. 20  Mwishowe Manase akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika+ katika nyumba yake; na Amoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 21  Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka miwili katika Yerusalemu.+ 22  Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kama alivyofanya Manase baba yake;+ na Amoni akatoa dhabihu+ kwa sanamu zote za kuchongwa+ ambazo Manase+ baba yake alikuwa ametengeneza, naye akaendelea kuzitumikia.+ 23  Naye hakujinyenyekeza+ kwa sababu ya Yehova kama Manase baba yake alivyojinyenyekeza,+ kwa maana Amoni ndiye aliyezidisha hatia.+ 24  Mwishowe watumishi wake wakampangia hila+ na kumuua ndani ya nyumba yake mwenyewe.+ 25  Lakini watu wa nchi wakawapiga na kuwaua+ wale wote waliompangia hila+ Mfalme Amoni,+ kisha watu+ wa nchi wakamfanya Yosia+ mwana wake kuwa mfalme mahali pake.

Maelezo ya Chini