2 Mambo ya Nyakati 32:1-33
32 Baada ya mambo hayo na mwendo huu wa uaminifu+ Senakeribu+ mfalme wa Ashuru+ akaja na kuvamia Yuda na kupiga kambi juu ya majiji yenye ngome,+ naye akaendelea kufikiria kuyafanya yawe yake kwa kuyavunja.
2 Hezekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na uso+ wake uko tayari kupiga vita juu ya Yerusalemu,
3 ndipo akaamua yeye pamoja na wakuu+ wake na wanaume wake wenye nguvu kuyaziba maji ya mabubujiko yaliyokuwa nje ya jiji;+ nao wakamsaidia.
4 Basi watu wengi wakakusanywa, nao wakaziba chemchemi zote na mto+ unaofurika kupitia katikati ya nchi, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kupata maji mengi?”
5 Tena akajipa moyo na kujenga ukuta wote uliovunjika+ na kusimamisha minara+ juu yake, na upande wa nje ukuta mwingine,+ akarekebisha Kilima+ cha Jiji la Daudi, na kutengeneza silaha+ kwa wingi na ngao.+
6 Naye akaweka wakuu wa majeshi+ juu ya watu na kuwakusanya kwake katika kiwanja cha watu wote+ cha lango la jiji na kusema na moyo+ wao, akiwaambia:
7 “Iweni hodari na wenye nguvu.+ Msiogope+ wala msiwe na hofu+ kwa sababu ya mfalme wa Ashuru+ na kwa sababu ya umati wote ulio pamoja naye;+ kwa maana kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja naye.
8 Yeye, mkono wa nyama uko pamoja naye,+ lakini sisi, Yehova Mungu wetu yuko pamoja nasi+ ili kutusaidia na kupigana vita vyetu.”+ Na watu wakaanza kujitegemeza juu ya maneno ya Hezekia mfalme wa Yuda.+
9 Baada ya hayo Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akawatuma watumishi wake mpaka Yerusalemu, wakati alipokuwa katika Lakishi+ pamoja na uwezo wake wote wa kifalme,+ kwenda kwa Hezekia mfalme wa Yuda na kwa Wayudea wote waliokuwa Yerusalemu, akisema:
10 “Senakeribu mfalme wa Ashuru amesema hivi,+ ‘Ni kitu gani mnachokitegemea huku mkiketi kimya katika Yerusalemu mkiwa mmezingirwa?+
11 Je, Hezekia+ siye anayewashawishi+ ninyi ili kuwatoa mfe kwa njaa na kwa kiu, akisema: “Yehova Mungu wetu atatukomboa kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru”?+
12 Je, Hezekia siye aliyeondoa mahali pa juu+ na madhabahu+ zake kisha akawaambia Yuda na Yerusalemu: “Mnapaswa kuinama+ mbele ya madhabahu moja+ nanyi mfukize juu yake moshi wa dhabihu”?+
13 Je, ninyi hamjui yale ambayo mimi mwenyewe na mababu zangu tulivitendea vikundi vyote vya watu wa nchi?+ Je, miungu+ ya mataifa ya zile nchi iliweza kukomboa hata kidogo nchi yao kutoka mkononi mwangu?
14 Kati ya miungu yote ya mataifa hayo ambayo mababu zangu waliangamiza ni nani aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu, hivi kwamba Mungu wenu aweze kuwakomboa ninyi kutoka mkononi mwangu?+
15 Na sasa msiache Hezekia awadanganye+ wala kuwashawishi+ ninyi hivyo wala msimwamini, kwa maana hakuna mungu yeyote wa taifa lolote au ufalme aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu na kutoka mkononi mwa mababu zangu. Basi, Mungu wenu atawezaje kuwakomboa ninyi kutoka mkononi mwangu!’”+
16 Na bado watumishi wake wakasema mabaya zaidi juu ya Yehova Mungu wa kweli,+ na juu ya Hezekia mtumishi wake.
17 Na hata akaandika barua+ za kumshutumu Yehova Mungu wa Israeli+ na kuongea vibaya juu yake, akisema: “Kama miungu+ ya mataifa ya nchi, ambayo haikuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu,+ vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hatawakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
18 Nao+ wakaendelea kuwaita watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta kwa sauti kubwa+ katika lugha ya Wayahudi+ ili kuwaogopesha+ na kuwatia wasiwasi, ili kwamba wapate kuliteka jiji.
19 Nao wakaendelea kusema vibaya+ juu ya Mungu wa Yerusalemu+ kama vile walivyofanya juu ya miungu ya vikundi vya watu wa dunia, iliyo kazi ya mikono ya mwanadamu.+
20 Lakini Hezekia+ mfalme na Isaya+ mwana wa Amozi,+ nabii,+ wakaendelea kusali kuhusu jambo hilo+ na kuendelea kuzililia mbingu ili kupata msaada.+
21 Na Yehova akamtuma malaika+ na kumfutilia mbali kila shujaa, mwanamume mwenye nguvu,+ na kiongozi na mkuu katika kambi ya mfalme wa Ashuru,+ hivi kwamba akarudi katika nchi yake akiwa na haya usoni. Baadaye akaingia katika nyumba ya mungu wake na humo watu fulani waliotoka katika viuno vyake mwenyewe wakamwangusha kwa upanga.+
22 Kwa hiyo Yehova akamwokoa Hezekia na wakaaji wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru+ na kutoka mkononi mwa wengine wote na kuwapa pumziko kuzunguka pande zote.+
23 Na kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakileta zawadi+ kwa Yehova katika Yerusalemu na vitu bora kwa Hezekia mfalme wa Yuda,+ naye akaja kuinuliwa+ machoni pa mataifa yote baada ya hayo.
24 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa kufikia hatua ya kufa,+ naye akaanza kusali+ kwa Yehova. Basi Yeye akasema naye,+ na Yeye akampa ishara.+
25 Lakini Hezekia hakurudisha kulingana na mema aliyotendewa,+ kwa kuwa moyo wake ulikuwa wenye majivuno+ na kukawa na ghadhabu+ juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
26 Hata hivyo, Hezekia akajinyenyekeza+ kwa sababu ya majivuno ya moyo wake, yeye pamoja na wakaaji wa Yerusalemu, na ghadhabu ya Yehova haikuja juu yao katika siku za Hezekia.+
27 Na Hezekia akawa na utajiri na utukufu kwa wingi sana;+ akajijengea maghala kwa ajili ya fedha na kwa ajili ya dhahabu+ na kwa ajili ya mawe ya thamani+ na kwa ajili ya mafuta ya zeri+ na kwa ajili ya ngao+ na kwa ajili ya vyombo vyote vyenye kutamanika;+
28 na pia maghala+ kwa ajili ya mazao ya nafaka na divai mpya+ na mafuta, na pia vibanda+ kwa ajili ya wanyama wote wa aina mbalimbali na vibanda kwa ajili ya makundi ya wanyama.
29 Naye akajipatia majiji, na pia wanyama wa kundi+ na wa mifugo+ kwa wingi; kwa maana Mungu alimpa mali nyingi sana.+
30 Na Hezekia ndiye aliyeziba+ chemchemi ya juu ya maji+ ya Gihoni+ na kuyaelekeza moja kwa moja chini upande wa magharibi mpaka Jiji la Daudi,+ na Hezekia akaendelea kufanikiwa katika kila moja ya kazi zake.+
31 Na hivyo ikawa kupitia wasemaji wa wakuu wa Babiloni+ waliotumwa kwake+ ili kuuliza habari za ile ishara+ iliyotendeka katika nchi, Mungu wa kweli akamwacha+ ili kumjaribu,+ apate kujua kila jambo lililokuwa moyoni mwake.+
32 Na yale mambo mengine+ ya Hezekia na matendo yake ya fadhili zenye upendo,+ tazama, yameandikwa katika maono ya Isaya nabii, mwana wa Amozi,+ katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na Israeli.
33 Mwishowe Hezekia akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika katika mpando wa kwenda kwenye makaburi ya wana wa Daudi;+ na Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakampa heshima wakati wa kifo chake.+ Na Manase+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.