2 Mambo ya Nyakati 31:1-21

31  Na mara tu walipomaliza hayo yote, Waisraeli+ wote waliokuwa hapo wakaenda katika majiji ya Yuda,+ nao wakazivunja nguzo takatifu+ na kuikata miti mitakatifu+ na kupabomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ kutoka katika Yuda+ yote na Benyamini na katika Efraimu+ na Manase+ mpaka walipomaliza; kisha wana wote wa Israeli wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.  Kisha Hezekia akaweka migawanyo+ ya makuhani na ya Walawi+ katika migawanyo yao, kila mmoja kulingana na utumishi wake kwa ajili ya makuhani+ na kwa ajili ya Walawi+ kuhusiana na toleo la kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika+ ili kuhudumu+ na kutoa shukrani+ na sifa+ katika malango ya kambi za Yehova.  Na kulikuwa na fungu la mfalme kutoka katika mali zake mwenyewe+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa,+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa ya asubuhi+ na jioni, na pia matoleo ya kuteketezwa kwa ajili ya sabato+ na kwa ajili ya miezi mipya+ na kwa ajili ya majira ya sherehe,+ kulingana na yaliyoandikwa katika sheria ya Yehova.+  Tena akawaambia watu, wakaaji wa Yerusalemu, kwamba watoe fungu la makuhani+ na la Walawi,+ ili waishike+ kabisa sheria ya Yehova.+  Na mara tu lile neno lilipoenea, wana wa Israeli+ wakazidisha mazao ya kwanza ya nafaka,+ divai mpya,+ na mafuta+ na asali+ na mazao yote ya shamba,+ nao wakaleta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+  Na wana wa Israeli na wa Yuda waliokuwa wakikaa katika majiji ya Yuda,+ wao wenyewe wakaleta sehemu ya kumi ya ng’ombe na kondoo na sehemu ya kumi ya vitu vitakatifu,+ vitu vilivyotakaswa kwa Yehova Mungu wao. Wakaleta, nao wakatoa mafungu juu ya mafungu.  Katika mwezi wa tatu+ walianzisha mafungu kwa kuweka tabaka ya chini zaidi, na katika mwezi wa saba+ wakamaliza.  Wakati Hezekia na wakuu+ walipokuja na kuona yale mafungu, wakambariki+ Yehova na watu wake Israeli.+  Baada ya muda Hezekia akawauliza makuhani na Walawi habari za yale mafungu.+ 10  Ndipo Azaria+ mkuu wa makuhani wa nyumba ya Sadoki+ akamwambia, ndiyo, akasema: “Tangu walipoanza kuleta mchango+ ndani ya nyumba ya Yehova kumekuwako kula na kushiba+ na kuwa na ziada kwa wingi;+ kwa kuwa Yehova mwenyewe amewabariki watu wake,+ na kilichobaki ni hiki kiasi kingi.” 11  Kwa hiyo Hezekia akasema vyumba vya kulia chakula+ vitayarishwe katika nyumba ya Yehova. Basi wakavitayarisha. 12  Nao wakaendelea kuleta ule mchango+ na ile sehemu ya kumi+ na vile vitu vitakatifu kwa uaminifu;+ na Konania Mlawi alikuwa akiwasimamia akiwa kiongozi, na Shimei ndugu yake alikuwa wa pili. 13  Na Yehieli na Azazia na Nahathi na Asaheli na Yerimothi na Yozabadi na Elieli na Ismakia na Mahathi na Benaya walikuwa wajumbe kando ya Konania na Shimei ndugu yake, kwa agizo la Hezekia mfalme, na Azaria+ alikuwa ndiye kiongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 14  Na Kore mwana wa Imna Mlawi alikuwa mtunza-lango+ upande wa mashariki,+ mwenye kusimamia matoleo ya hiari+ ya Mungu wa kweli, ili kutoa mchango+ wa Yehova na vitu vitakatifu zaidi.+ 15  Na chini yake palikuwa na Edeni na Miniamini na Yeshua na Shemaya, Amaria na Shekania, katika majiji ya makuhani,+ katika vyeo vyenye kutegemeka,+ ili kuwapa ndugu zao katika migawanyo,+ wakubwa na wadogo kwa kiwango sawasawa;+ 16  mbali na maandikisho ya kiukoo+ ya wanaume wenye umri wa kuanzia miaka mitatu na zaidi,+ kati ya wale wote wanaoingia katika nyumba ya Yehova kama desturi ya kila siku, kwa ajili ya utumishi wao kulingana na wajibu wao kufuatana na migawanyo yao. 17  Huu ndio uandikisho wa kiukoo wa makuhani kulingana na nyumba za baba+ zao na pia za Walawi,+ kuanzia umri wa miaka 20+ na zaidi, kulingana na wajibu wao katika migawanyo+ yao; 18  kwa ajili ya uandikisho wa kiukoo kati ya watoto wao wote, wake zao na wana wao na binti zao, kwa ajili ya kutaniko lote, kwa sababu walijitakasa+ katika vyeo vyao vyenye kutegemeka+ kwa ajili ya kilicho kitakatifu; 19  na kwa ajili ya wana wa Haruni,+ makuhani, katika mashamba ya viwanja+ vya malisho vya majiji yao. Katika majiji yote mbalimbali kulikuwa na watu waliowekwa kulingana na majina yao, ili kumpa mafungu kila mwanamume kati ya makuhani na kwa uandikisho wote wa kiukoo kati ya Walawi. 20  Na Hezekia akafanya hivyo katika Yuda yote, naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mema+ na sawa+ na yenye uaminifu+ mbele za Yehova Mungu wake. 21  Na katika kila kazi aliyoanza katika utumishi+ wa nyumba ya Mungu wa kweli na katika sheria+ na katika amri ili kumtafuta+ Mungu wake, alitenda kwa moyo wake wote,+ naye akafanikiwa.+

Maelezo ya Chini