2 Mambo ya Nyakati 30:1-27

30  Na Hezekia akatuma ujumbe kwa Israeli+ wote na Yuda, na hata akaandika barua kwa Efraimu+ na Manase,+ waje Yerusalemu katika nyumba ya Yehova+ ili kumfanyia pasaka+ Yehova Mungu wa Israeli.  Hata hivyo, mfalme na wakuu+ wake na kutaniko+ lote katika Yerusalemu wakaazimia kufanya pasaka katika mwezi wa pili;+  kwa maana hawakuweza kuifanya wakati huo,+ kwa sababu makuhani+ wa kutosha hawakuwa wamejitakasa na watu hawakuwa wamekusanyika Yerusalemu.  Na jambo hilo lilikuwa sawa machoni pa mfalme na machoni pa kutaniko lote.+  Basi wakaamua kueneza mwito+ huo katika Israeli yote, kuanzia Beer-sheba+ mpaka Dani,+ ili waje na kufanya pasaka kwa Yehova Mungu wa Israeli katika Yerusalemu; kwa maana hawakuwa wamefanya hivyo+ wakiwa umati kulingana na yale ambayo yameandikwa.+  Kwa hiyo wakimbiaji+ walio na zile barua kutoka katika mkono wa mfalme na wa wakuu+ wake wakaenda katika Israeli yote na Yuda, kulingana na amri ya mfalme, na kusema: “Ninyi wana wa Israeli, rudini+ kwa Yehova Mungu+ wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili yeye arudi kwa wale walioponyoka+ ambao wamebaki kati yenu kutoka katika mkono wa wafalme wa Ashuru.+  Na msiwe kama mababu zenu+ na kama ndugu zenu waliotenda kwa ukosefu wa uaminifu kumwelekea Yehova Mungu wa mababu zao, hivi kwamba akawafanya kuwa kitu cha kushangaza,+ kama vile mnavyoona.  Sasa msifanye shingo+ zenu kuwa ngumu kama walivyofanya mababu zenu. Mpeni Yehova nafasi+ na mje katika patakatifu pake+ ambapo amepatakasa+ mpaka wakati usio na kipimo na kumtumikia+ Yehova Mungu wenu, ili hasira yake inayowaka+ iondoke kwenu.  Kwa maana wakati mtakaporudi+ kwa Yehova, ndugu zenu na wana wenu wataonyeshwa rehema+ mbele ya wale wanaowashika mateka, na kuruhusiwa kurudi katika nchi hii;+ kwa kuwa Yehova Mungu wenu, ni mwenye neema+ na rehema,+ wala hatageuza uso kutoka kwenu mkirudi kwake.”+ 10  Kwa hiyo wale wakimbiaji+ wakaendelea, wakapita jiji baada ya jiji katika nchi yote ya Efraimu+ na Manase, mpaka Zabuloni; lakini wakaendelea kuwafanyia mzaha na kuwadharau.+ 11  Ni watu mmoja mmoja+ tu kutoka Asheri na Manase na kutoka Zabuloni waliojinyenyekeza,+ hivi kwamba wakaja Yerusalemu. 12  Mkono wa Mungu wa kweli ukawa katika Yuda pia ili kuwapa moyo mmoja+ ili watende amri+ ya mfalme na wakuu kuhusu lile jambo la Yehova.+ 13  Nao wakakusanyika Yerusalemu,+ watu wengi sana, ili kufanya sherehe+ ya keki zisizo na chachu katika mwezi wa pili,+ kutaniko lenye watu wengi sana. 14  Kisha wakasimama na kuziondoa madhabahu+ zilizokuwa Yerusalemu, wakaziondoa madhabahu+ zote za uvumba, nao wakazitupa katika bonde la mto la Kidroni.+ 15  Kisha wakachinja mnyama wa pasaka+ katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili; na makuhani na Walawi walikuwa wametiwa aibu, hivi kwamba wakajitakasa+ na kuleta matoleo ya kuteketezwa kwenye nyumba ya Yehova. 16  Nao wakaendelea kusimama+ mahali pao kulingana na kanuni yao, kulingana na sheria ya Musa yule mtu wa Mungu wa kweli, makuhani+ wakinyunyiza damu iliyopokewa kutoka mkononi mwa Walawi. 17  Kwa maana palikuwa na wengi katika kutaniko ambao hawakuwa wamejitakasa; na Walawi+ walikuwa wakisimamia kuchinjwa kwa wanyama wa pasaka+ kwa ajili ya wote ambao hawakuwa safi, ili kuwatakasa kwa Yehova. 18  Kwa maana palikuwa na hesabu kubwa ya watu, wengi kutoka Efraimu+ na Manase,+ Isakari na Zabuloni,+ ambao hawakuwa wamejitakasa,+ kwa maana hawakula pasaka kulingana na yale ambayo yameandikwa;+ lakini Hezekia akasali kwa ajili yao,+ na kusema: “Yehova aliye mwema+ na amkubali 19  kila mtu ambaye ameutayarisha moyo+ wake ili kumtafuta Mungu wa kweli, Yehova Mungu wa mababu zake, ingawa hajatakaswa kwa ajili ya kilicho kitakatifu.”+ 20  Basi Yehova akamsikiliza Hezekia na kuwaponya watu.+ 21  Hivyo wana wa Israeli waliokuwa Yerusalemu wakafanya sherehe+ ya keki zisizo na chachu kwa siku saba kwa shangwe kubwa;+ na Walawi+ na makuhani+ walikuwa wakimtolea Yehova sifa siku baada ya siku kwa vyombo vyenye sauti kubwa, naam, kwa Yehova.+ 22  Tena Hezekia akasema kwa moyo+ wa Walawi wote waliokuwa wakitenda kwa busara njema kumwelekea Yehova.+ Nao wakala sherehe rasmi kwa siku saba,+ wakitoa dhabihu za ushirika+ na kuungama+ kwa Yehova Mungu wa mababu zao. 23  Kisha kutaniko lote likaamua+ kuifanya kwa siku saba zaidi,+ basi wakaifanya kwa siku saba kwa kushangilia. 24  Kwa maana Hezekia mfalme wa Yuda alichanga+ kwa ajili ya kutaniko ng’ombe elfu moja na kondoo elfu saba, na wakuu+ wakachanga kwa ajili ya kutaniko ng’ombe elfu moja na kondoo elfu kumi; na hesabu kubwa ya makuhani+ wakaendelea kujitakasa. 25  Na kutaniko lote la Yuda+ na makuhani na Walawi+ na kutaniko lote lililokuja kutoka katika Israeli+ na wakaaji wageni+ waliokuja kutoka katika nchi ya Israeli+ na wale wanaokaa Yuda wakaendelea kushangilia.+ 26  Na kukawa na shangwe kubwa Yerusalemu, kwa maana tangu siku za Sulemani+ mwana wa Daudi mfalme wa Israeli hakukuwa na shangwe kama hiyo katika Yerusalemu.+ 27  Mwishowe makuhani, Walawi, wakasimama na kuwabariki+ watu; na sauti yao ikasikilizwa, hivi kwamba sala yao ikaingia katika makao yake matakatifu, mbinguni.+

Maelezo ya Chini