2 Mambo ya Nyakati 3:1-17
3 Mwishowe Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria,+ ambapo Yehova alikuwa amemtokea Daudi baba yake,+ mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani+ Myebusi.
2 Basi akaanza kujenga katika mwezi wa pili, siku ya pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.+
3 Na vitu hivi Sulemani akaviweka kuwa msingi kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu wa kweli, urefu wa kipimo cha mikono kulingana na kipimo cha zamani ukiwa mikono 60, na upana mikono 20.+
4 Na ukumbi+ uliokuwa mbele ya huo urefu ulikuwa mikono 20 mbele ya upana wa nyumba, na kimo chake kilikuwa 120; naye akafunika upande wa ndani kwa dhahabu safi.
5 Na ile nyumba kuu+ akaifunika kwa miberoshi, kisha akaifunika kwa dhahabu nzuri,+ halafu akaweka juu yake maumbo ya mtende+ na minyororo.+
6 Tena, akaitandaza nyumba kwa mawe ya thamani kwa ajili ya uzuri;+ na dhahabu+ ilikuwa dhahabu ya kutoka katika nchi ya dhahabu.
7 Naye akafunika kwa dhahabu ile nyumba, maboriti, vizingiti na kuta zake na milango yake;+ akachonga makerubi juu ya kuta.+
8 Naye akajenga nyumba ya Patakatifu Zaidi,+ urefu wake kuhusiana na upana wa nyumba ulikuwa mikono 20, na upana wake ulikuwa mikono 20;+ kisha akaifunika kwa dhahabu nzuri kiasi chake talanta 600.
9 Na uzito wa misumari+ ulikuwa shekeli 50 za dhahabu; naye akavifunika vyumba vya dari kwa dhahabu.
10 Kisha akatengeneza makerubi+ wawili katika nyumba ya Patakatifu Zaidi kwa kutumia ufundi wa kufanya mifano, akawafunika kwa dhahabu.+
11 Na urefu wa mabawa ya wale makerubi+ ulikuwa mikono 20, bawa moja la urefu wa mikono 5 lilifika kwenye ukuta wa nyumba ile, na lile bawa lingine la urefu wa mikono 5 likiwa linafika kwenye bawa la yule kerubi mwingine.+
12 Na bawa la yule kerubi mmoja la urefu wa mikono 5 lilikuwa linafika kwenye ukuta wa nyumba ile, na lile bawa lingine la mikono 5 lilishikana na bawa la yule kerubi mwingine.+
13 Mabawa ya hao makerubi yalikuwa yamenyooshwa urefu wa mikono 20; nao walikuwa wamesimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea upande wa ndani.
14 Tena akatengeneza pazia+ la uzi wa bluu+ na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na uzi mwekundu na kitambaa laini, na kulipamba kwa makerubi juu yake.+
15 Kisha akatengeneza nguzo mbili+ mbele ya nyumba ile, urefu wa mikono 35, na kombe+ lililokuwa juu ya kila moja lilikuwa na urefu wa mikono 5.
16 Tena, akatengeneza minyororo+ yenye mtindo wa mkufu na kuiweka juu ya vilele vya zile nguzo, akatengeneza makomamanga+ mia moja na kuyaweka kwenye ile minyororo.
17 Naye akasimamisha zile nguzo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume na nyingine upande wa kushoto, kisha ile ya upande wa kuume akaiita jina Yakini na jina la ile ya upande wa kushoto Boazi.+