2 Mambo ya Nyakati 26:1-23

26  Ndipo watu+ wote wa Yuda wakamchukua Uzia,+ akiwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya+ kuwa mfalme mahali pa Amazia+ baba yake.  Yeye ndiye aliyejenga upya Elothi+ kisha akalirudisha kwa Yuda baada ya mfalme kulala pamoja na mababu zake.+  Uzia+ alianza kutawala akiwa na umri wa miaka 16, naye akatawala miaka 52 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yekolia+ wa Yerusalemu.  Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kulingana na yote ambayo Amazia baba yake alikuwa amefanya.+  Naye akaendelea kuwa na mwelekeo wa kumtafuta+ Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa akiwafundisha watu kumwogopa Mungu wa kweli;+ na katika zile siku alizokuwa akimtafuta Yehova, Mungu wa kweli alimfanikisha.+  Naye akatoka kwenda kupigana na Wafilisti,+ akapenya ukuta wa Gathi+ na ukuta wa Yabne+ na ukuta wa Ashdodi,+ kisha akajenga majiji katika eneo la Ashdodi+ na katikati ya Wafilisti.  Na Mungu wa kweli akaendelea kumsaidia+ juu ya Wafilisti na juu ya Waarabu+ waliokuwa wakikaa katika Gurbaali na Meunimu.+  Na Waamoni+ wakaanza kumpa Uzia ushuru.+ Mwishowe sifa+ yake ikaenea mpaka Misri, kwa kuwa alionyesha nguvu kwa kiwango kisicho cha kawaida.  Zaidi ya hayo, Uzia akajenga minara+ katika Yerusalemu kando ya Lango la Pembeni+ na kando ya Lango la Bonde+ na kando ya Nguzo, naye akaitia nguvu. 10  Tena akajenga minara+ nyikani, na kuchimba matangi mengi ya maji (kwa maana alikuwa na mifugo mingi sana), na pia katika Shefela+ na katika nchi tambarare ya juu. Palikuwa na wakulima na watunza-mizabibu katika milima na katika Karmeli, kwa maana alipenda kilimo. 11  Tena Uzia akawa na jeshi la kupigana vita, wale wanaoingia katika utumishi wa kijeshi vikosi vikosi,+ kulingana na hesabu ya uandikisho+ wao kwa mkono wa Yeieli mwandishi+ na Maaseya ofisa aliye chini ya+ Hanania mmoja wa wakuu wa mfalme.+ 12  Hesabu kamili ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ ya mashujaa,+ wanaume wenye nguvu,+ ilikuwa elfu mbili na mia sita. 13  Na chini ya amri yao majeshi yalikuwa ni watu mia tatu na saba elfu na mia tano wa kupigana vita wakiwa na nguvu za kijeshi ili kumsaidia mfalme kupigana na adui.+ 14  Na Uzia akaendelea kuwafanyia matayarisho, jeshi lote, ngao+ na mikuki+ na kofia+ na mavazi ya chuma+ na pinde+ na mawe ya kombeo.+ 15  Tena akatengeneza mitambo ya vita katika Yerusalemu, ubuni wa mafundi, ili iwekwe juu ya minara+ na juu ya sehemu za pembeni, ili irushe mishale na mawe makubwa. Basi sifa+ yake ikaenea mbali sana, kwa kuwa alisaidiwa kwa njia ya ajabu mpaka akawa na nguvu. 16  Hata hivyo, mara tu alipopata nguvu, moyo wake ukawa na majivuno+ hata kufikia hatua ya kusababisha uharibifu,+ hivi kwamba akatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa Yehova Mungu wake, akaingia katika hekalu la Yehova ili kufukiza uvumba juu ya madhabahu ya uvumba.+ 17  Mara moja Azaria kuhani na makuhani wa Yehova pamoja naye, wanaume mashujaa 80, wakaingia nyuma yake. 18  Kisha wakasimama kumpinga Uzia mfalme+ na kumwambia: “Si kazi yako,+ Ee Uzia, kumfukizia Yehova uvumba, bali ni kazi ya makuhani, wana wa Haruni,+ waliotakaswa, kufukiza uvumba. Ondoka ndani ya patakatifu; kwa maana umetenda kwa ukosefu wa uaminifu, wala jambo hilo si utukufu+ wowote kwako mbele za Yehova Mungu.” 19  Lakini Uzia akawa na ghadhabu,+ huku mkononi mwake akiwa na chetezo,+ cha kufukiza uvumba, na, alipokuwa na ghadhabu juu ya makuhani, ukoma+ ukatokea+ katika paji la uso wake mbele ya wale makuhani katika nyumba ya Yehova kando ya madhabahu ya uvumba. 20  Wakati Azaria yule mkuu wa makuhani na makuhani wote walipogeuka kumwelekea, tazama, alikuwa amepigwa na ukoma katika paji la uso wake!+ Kwa hiyo wakaanza kumtoa hapo upesi, naye mwenyewe pia akafanya haraka kutoka nje, kwa sababu Yehova alikuwa amempiga.+ 21  Na Uzia+ mfalme akaendelea kuwa mwenye ukoma mpaka siku ya kufa kwake, naye akaendelea kukaa katika nyumba fulani akiwa ameondolewa wajibu wake, akiwa mwenye ukoma;+ kwa sababu alikuwa ametengwa na nyumba ya Yehova, huku Yothamu mwana wake akiwa juu ya nyumba ya mfalme, akiwahukumu watu wa nchi. 22  Na yale mambo mengine ya Uzia,+ ya kwanza na ya mwisho, Isaya+ mwana wa Amozi+ nabii ameyaandika. 23  Mwishowe Uzia akalala pamoja na mababu zake; na kwa hiyo wakamzika pamoja na mababu zake, lakini katika uwanja wa kuzikia wa wafalme,+ kwa maana walisema: “Yeye ni mwenye ukoma.” Na Yothamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

Maelezo ya Chini