2 Mambo ya Nyakati 25:1-28
25 Amazia+ alikuwa mfalme akiwa na umri wa miaka 25, naye akatawala miaka 29 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yehoadani+ wa Yerusalemu.
2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ ila tu si kwa moyo kamili.+
3 Na ikawa kwamba mara tu ufalme ulipokuwa umeimarishwa kwake, akawaua+ mara moja wale watumishi+ wake waliompiga na kumuua mfalme, baba yake.+
4 Naye hakuwaua wana wao, bali alifanya kulingana na yale ambayo yameandikwa katika sheria, katika kitabu cha Musa,+ ambayo Yehova aliamuru, akisema: “Akina baba wasife kwa sababu ya wana,+ wala wana wasife kwa sababu ya akina baba;+ bali kila mmoja afe kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+
5 Na Amazia akawakusanya Yuda na kuwasimamisha kulingana na nyumba ya mababu,+ kulingana na wakuu wa maelfu+ na kulingana na wakuu wa mamia+ kwa ajili ya Yuda wote na Benyamini; naye akawaandikisha kuanzia umri wa miaka 20+ na zaidi, na mwishowe akakuta kwamba walikuwa wanaume bora 300,000 wanaoingia jeshini, wanaotumia mkuki+ na ngao kubwa.+
6 Tena akaandika kutoka katika Israeli mashujaa, wanaume wenye nguvu mia moja elfu kwa talanta mia moja za fedha.
7 Na mtu fulani wa Mungu wa kweli+ akamjia, akisema: “Ee mfalme, usiache jeshi la Israeli liende pamoja nawe, kwa maana Yehova hayuko pamoja na Israeli,+ yaani, wana wote wa Efraimu.
8 Lakini wewe mwenyewe nenda, utende, uwe hodari kwa ajili ya vita.+ Mungu wa kweli anaweza kukufanya ujikwae mbele ya adui; kwa maana Mungu ana nguvu za kusaidia+ na za kusababisha kujikwaa.”+
9 Ndipo Amazia+ akamwambia yule mtu wa Mungu wa kweli: “Lakini zifanyweje zile talanta mia moja ambazo nimewapa majeshi ya Israeli?”+ Mtu wa Mungu wa kweli akajibu, akasema: “Yehova ana uwezo wa kukupa nyingi zaidi kuliko hizo.”+
10 Basi Amazia akawatenga, yaani, yale majeshi yaliyomjia kutoka Efraimu, ili waende kwao. Hata hivyo, hasira yao ikawaka sana juu ya Yuda, nao wakarudi kwao wakiwaka hasira.+
11 Naye Amazia akajipa moyo, akawaongoza watu wake, akaenda katika Bonde la Chumvi;+ naye akawapiga wana wa Seiri,+ elfu kumi kati yao.+
12 Na wana wa Yuda wakakamata watu elfu kumi wakiwa hai. Basi wakawaleta kwenye kilele cha mwamba, wakawatupa kutoka kilele cha mwamba ule; nao wote wakapasuka.+
13 Na wale askari-jeshi ambao Amazia alirudisha wasiende pamoja naye vitani,+ wakaanza kuvamia majiji ya Yuda, kuanzia Samaria+ mpaka Beth-horoni,+ wakawapiga elfu tatu kati yao na kuchukua nyara nyingi.
14 Lakini ikawa kwamba baada ya Amazia kurudi kutoka kuwapiga Waedomu, akaleta miungu+ ya wana wa Seiri na kujisimamishia iwe miungu,+ naye akaanza kuinama mbele yake,+ naye akaanza kuifukizia moshi wa dhabihu.+
15 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Amazia, na hivyo akamtumia nabii na kumwambia: “Kwa nini umeitafuta+ miungu ya watu+ ambayo haikuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwako?”+
16 Na ikawa kwamba aliposema naye, mara moja mfalme akamwambia: “Je, tulikuweka wewe kuwa mshauri wa mfalme?+ Acha kwa faida yako mwenyewe.+ Kwa nini wakupige na kukuua?” Kwa hiyo yule nabii akaacha, lakini akasema: “Hakika ninajua kwamba Mungu ameazimia kukuangamiza wewe,+ kwa sababu umetenda hivi+ wala hukulisikiliza shauri langu.”+
17 Na Amazia mfalme wa Yuda akatafuta shauri na kutuma ujumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli,+ na kusema: “Njoo! Tutazamane uso kwa uso.”+
18 Ndipo Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma ujumbe kwa Amazia mfalme wa Yuda, na kusema:+ “Gugu lenye miiba lililokuwa katika Lebanoni lilituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa katika Lebanoni,+ na kusema, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’+ Hata hivyo, mnyama wa mwituni+ aliyekuwa katika Lebanoni akapita karibu, akalikanyaga lile gugu lenye miiba.
19 Umesema moyoni mwako, Tazama, umepiga Edomu.+ Na moyo+ wako umekuinua ili utukuzwe.+ Sasa endelea kukaa nyumbani kwako mwenyewe.+ Kwa nini ujiingize katika mzozo katika hali zisizofaa+ hata uanguke, wewe na Yuda pamoja nawe?”+
20 Lakini Amazia hakusikiliza; kwa maana jambo hilo lilitoka kwa Mungu wa kweli+ kwa kusudi la kuwatia mkononi mwake, kwa sababu walikuwa wameitafuta miungu ya Edomu.+
21 Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akapanda,+ nao wakatazamana uso kwa uso,+ yeye na Amazia mfalme wa Yuda, kule Beth-shemeshi,+ ya Yuda.
22 Na Yuda wakashindwa mbele ya Israeli,+ hata wakaanza kukimbia, kila mmoja kwenda katika hema lake.+
23 Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akamkamata+ Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, kule Beth-shemeshi, kisha akamleta Yerusalemu,+ naye akabomoa shimo katika ukuta wa Yerusalemu, kuanzia Lango la Efraimu+ mpaka kwenye Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono mia nne.
24 Naye akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika nyumba ya Mungu wa kweli na Obed-edomu+ na hazina za nyumba ya mfalme+ na mateka, kisha akarudi Samaria.+
25 Na Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda akaendelea kuishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+
26 Na mambo mengine ya Amazia, ya kwanza na ya mwisho,+ tazama! je, hayakuandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na Israeli?+
27 Na kutoka wakati Amazia alipogeuka akaacha kumfuata Yehova, wakapanga hila+ juu yake katika Yerusalemu. Mwishowe akakimbilia Lakishi;+ lakini wakatuma watu kumfuatilia huko Lakishi, wakamuua huko.+
28 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi,+ wakamzika pamoja na mababu zake katika jiji la Yuda.+