2 Mambo ya Nyakati 23:1-21
23 Na katika mwaka wa saba Yehoyada+ akajionyesha kuwa hodari, akawachukua wakuu wa mamia,+ yaani, Azaria mwana wa Yerohamu, na Ishmaeli mwana wa Yehohanani na Azaria mwana wa Obedi na Maaseya mwana wa Adaya na Elishafati mwana wa Zikri, pamoja naye katika agano.
2 Kisha wakazunguka Yuda yote na kuwakusanya Walawi+ kutoka katika majiji yote ya Yuda na vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za Israeli. Basi wakaja Yerusalemu.
3 Ndipo kutaniko lote wakafanya agano+ pamoja na mfalme katika nyumba+ ya Mungu wa kweli, kisha akawaambia:
“Tazama! Mwana+ wa mfalme atatawala,+ kama Yehova alivyoahidi kuhusiana na wana wa Daudi.+
4 Hivi ndivyo mtakavyofanya: sehemu ya tatu kati yenu mnaoingia siku ya sabato,+ ya makuhani+ na ya Walawi,+ watakuwa watunza-milango;+
5 na sehemu ya tatu watakuwa katika nyumba ya mfalme;+ na sehemu ya tatu watakuwa kwenye Lango la Msingi;+ na watu wote watakuwa katika nyua+ za nyumba ya Yehova.
6 Na msimruhusu mtu yeyote aingie katika nyumba ya Yehova+ ila makuhani na wale Walawi wanaohudumu.+ Hao ndio watakaoingia, kwa sababu wao ni kikundi kitakatifu,+ na watu wote watashika huo wajibu kwa Yehova.
7 Na Walawi wanapaswa kumzunguka mfalme pande zote,+ kila mmoja akiwa na silaha zake mkononi mwake; na mtu yeyote atakayeingia ndani ya nyumba, anapaswa kuuawa. Nanyi mwendelee kuwa na mfalme anapoingia ndani na anapotoka nje.”
8 Na wale Walawi na Yuda wote wakafanya kulingana na yote ambayo Yehoyada+ kuhani alikuwa ameamuru.+ Basi kila mmoja wao akachukua watu wake waliokuwa wakiingia wakati wa sabato pamoja na wale waliokuwa wakitoka nje wakati wa sabato,+ kwa kuwa Yehoyada kuhani hakuwa ameviachisha kazi vile vikundi vya migawanyo.+
9 Tena Yehoyada kuhani akawapa wale wakuu wa mamia+ mikuki na ngao na ngao za mviringo+ zilizokuwa za Mfalme Daudi,+ ambazo zilikuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli.+
10 Naye akawasimamisha watu wote,+ kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, kuanzia upande wa kuume wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu na kando ya nyumba, pande zote karibu na mfalme.
11 Kisha wakamtoa nje mwana wa mfalme,+ wakamvika taji+ na ule Ushuhuda,+ wakamfanya kuwa mfalme, hivyo Yehoyada na wanawe wakamtia mafuta+ na kusema: “Mfalme na aishi!”+
12 Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia na kumsifu mfalme,+ mara moja akaingia kwa watu katika nyumba ya Yehova.
13 Kisha akaona, na tazama, mfalme alikuwa amesimama kando ya nguzo+ yake katika mwingilio, na wakuu+ na tarumbeta+ kando ya mfalme, na watu wote wa nchi walikuwa wakishangilia+ na kupiga+ tarumbeta, na waimbaji+ walikuwa na vyombo vya nyimbo na wale wanaotoa ishara za kutoa sifa. Athalia akayararua mavazi yake mara moja na kusema: “Ni hila! Ni hila!”+
14 Lakini Yehoyada kuhani akawatoa nje wale wakuu wa mamia, watu waliochaguliwa wa jeshi, na kuwaambia: “Mwondoeni katikati ya vikosi;+ na yeyote atakayemfuata, auawe kwa upanga!” Kwa maana kuhani yule alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.”
15 Basi wakamkamata. Alipofika katika mwingilio wa lango la farasi la nyumba ya mfalme, wakamuua hapo mara moja.+
16 Ndipo Yehoyada akafanya agano kati yake na watu wote na mfalme kwamba wao wataendelea kuwa watu+ wa Yehova.
17 Kisha watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Baali, wakaibomoa;+ nao wakazivunja madhabahu+ zake na sanamu+ zake, nao, mbele ya zile madhabahu, wakamuua+ Matani+ kuhani wa Baali.
18 Tena Yehoyada akavitia vyeo vya nyumba ya Yehova mkononi mwa makuhani na Walawi, ambao Daudi+ alikuwa amewaweka katika migawanyo juu ya nyumba ya Yehova ili watoe dhabihu za kuteketezwa za Yehova kulingana na yale ambayo yameandikwa katika sheria ya Musa,+ kwa kushangilia pamoja na nyimbo kwa mikono ya Daudi.
19 Kwa hiyo akawaweka watunza-malango+ kando ya malango+ ya nyumba ya Yehova ili yeyote aliye najisi katika jambo lolote asiingie.
20 Sasa akawachukua wakuu wa mamia+ na mabwana na watawala juu ya watu na watu wote wa nchi na kumshusha mfalme kutoka katika nyumba ya Yehova.+ Kisha wakaja moja kwa moja kupitia lango la juu mpaka kwenye nyumba ya mfalme, wakamketisha mfalme juu ya kiti cha ufalme.+
21 Na watu wote wa nchi wakaendelea kushangilia;+ nalo jiji halikuwa na usumbufu, nao walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga.+