2 Mambo ya Nyakati 20:1-37
20 Na ikawa kwamba baadaye wana wa Moabu+ na wana wa Amoni+ na pamoja nao baadhi ya Waamonimu+ wakaja kupigana vita na Yehoshafati.+
2 Basi watu wakaja na kumwambia Yehoshafati, wakisema: “Umati mkubwa umekuja kukushambulia kutoka katika eneo la bahari, kutoka Edomu;+ na, tazama, wako huko Hasason-tamari, yaani, En-gedi.”+
3 Ndipo Yehoshafati akaogopa,+ akauelekeza uso wake kumtafuta Yehova.+ Kwa hiyo akatangaza mfungo+ kwa ajili ya Yuda yote.
4 Mwishowe watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kuuliza habari kutoka kwa Yehova.+ Wakaja kutoka katika majiji yote ya Yuda ili kutafuta shauri kwa Yehova.+
5 Ndipo Yehoshafati akasimama katika kutaniko la Yuda na la Yerusalemu ndani ya nyumba ya Yehova+ mbele ya ule ua mpya,+
6 naye akasema:+
“Ee Yehova Mungu wa mababu zetu,+ je, wewe si Mungu mbinguni,+ na je, wewe hutawali juu ya falme zote za mataifa,+ na je, mkononi mwako hamna nguvu na uwezo, wala hakuna anayeweza kusimama imara kupingana nawe?+
7 Je, wewe mwenyewe, Ee Mungu wetu,+ hukuwafukuza wakaaji wa nchi hii kutoka mbele ya watu wako Israeli,+ kisha ukaikabidhi+ kwa uzao wa Abrahamu, mpendwa wako,+ mpaka wakati usio na kipimo?
8 Nao wakaanza kukaa ndani yake, nao wakakujengea patakatifu ndani yake kwa ajili ya jina lako,+ wakisema,
9 ‘Tukipatwa na msiba,+ upanga, hukumu mbaya, au tauni+ au njaa,+ acheni tusimame mbele ya nyumba hii+ na mbele zako (kwa maana jina lako+ limo katika nyumba hii), ili tukuombe msaada ili kutuondoa katika taabu yetu, nawe usikie na kuokoa.’+
10 Na sasa, tazama, wana wa Amoni,+ na Moabu+ na eneo lenye milima la Seiri,+ ambao hukuruhusu Israeli wawavamie walipokuwa wakitoka katika nchi ya Misri, bali waligeukia mbali kutoka kwao wala hawakuwaangamiza,+
11 ndiyo, tazama, wanatupa sisi thawabu+ ya kuja kutufukuza tuondoke katika miliki yako ambayo ulitufanya tuimiliki.+
12 Ee Mungu wetu, je, hutafanya hukumu juu yao?+ Kwa maana hakuna nguvu ndani yetu mbele ya umati huu mkubwa unaokuja juu yetu;+ nasi wenyewe hatujui tunalopaswa kufanya,+ lakini macho yetu yanakuelekea wewe.”+
13 Na wakati huo wote watu wote wa Yuda walikuwa wamesimama mbele za Yehova,+ hata watoto wao,+ wake zao na wana wao.
14 Sasa kwa habari ya Yahazieli mwana wa Zekaria mwana wa Benaya mwana wa Yeieli mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu,+ roho+ ya Yehova ikaja juu yake katikati ya kutaniko.
15 Basi akasema: “Sikilizeni kwa makini, Yuda wote nanyi wakaaji wa Yerusalemu na Mfalme Yehoshafati! Tazama, Yehova amewaambia ninyi hivi, ‘Msiogope+ wala msiwe na hofu kwa sababu ya umati huu mkubwa; kwa maana vita si vyenu bali ni vya Mungu.+
16 Washukieni kesho. Tazama, wanapanda kuja kwa njia nyembamba ya Sisi; nanyi hakika mtawakuta mwishoni mwa bonde la mto mbele ya nyika ya Yerueli.
17 Hamtahitaji kupigana+ katika kisa hiki. Simameni mahali penu, simameni tuli,+ mkauone wokovu+ wa Yehova kwa ajili yenu. Ee Yuda na Yerusalemu, msiogope wala msiwe na hofu.+ Kesho waendeeni, na Yehova atakuwa pamoja nanyi.’”+
18 Ndipo mara moja Yehoshafati akainama kifudifudi,+ na Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakaanguka mbele za Yehova ili kumsujudia Yehova.+
19 Kisha Walawi+ wa wana wa Wakohathi+ na wa wana wa Wakora+ wakasimama ili kumsifu Yehova Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa isivyo kawaida.+
20 Nao wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda katika nyika+ ya Tekoa.+ Na walipokuwa wakienda, Yehoshafati akasimama na kusema: “Nisikieni, enyi Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu!+ Iweni na imani+ katika Yehova Mungu wenu, ili mdumu muda mrefu. Iweni na imani katika manabii wake,+ hivyo mfanikiwe.”
21 Tena akafanya shauri+ na watu na kuweka waimbaji+ kwa ajili ya Yehova na wale wanaotoa sifa+ katika pambo takatifu+ wakienda mbele ya wale watu wenye silaha,+ na kusema: “Mpeni Yehova sifa,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
22 Na wakati walipoanza kupaaza vigelegele vya shangwe na sifa, Yehova akaweka watu wa kuvizia+ juu ya wana wa Amoni, Moabu na eneo lenye milima la Seiri waliokuwa wakija Yuda, nao wakaanza kupigana wenyewe.+
23 Na wana wa Amoni na Moabu wakasimama kushambulia wakaaji wa eneo lenye milima la Seiri+ ili kuwaangamiza na kuwaharibu; na mara tu walipowamaliza wakaaji wa Seiri, wakasaidiana kuangamizana wao kwa wao.+
24 Lakini Yuda wakaja kwenye mnara wa mlinzi wa nyika.+ Walipogeuza nyuso zao kuelekea ule umati, tazama, pale, mizoga yao ikiwa imeanguka chini+ bila yeyote kuponyoka.
25 Basi Yehoshafati na watu wake wakaja kupora nyara+ walizokuwa nazo, na katika nyara hizo wakakuta kwa wingi mali na mavazi na vyombo vyenye kutamanika; nao wakaendelea kuwavua mpaka waliposhindwa kuchukua zaidi.+ Nao wakapora nyara kwa siku tatu, kwa maana zilikuwa nyingi.
26 Na katika siku ya nne wakakutana pamoja kwenye nchi tambarare ya chini ya Baraka, kwa maana walimbariki Yehova hapo.+ Ndiyo sababu walipaita mahali hapo jina+ Nchi Tambarare ya Chini ya Baraka—mpaka leo hii.
27 Ndipo watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakarudi, Yehoshafati akiwa mbele yao, ili warudi Yerusalemu kwa kushangilia, kwa kuwa Yehova alikuwa amewafanya washangilie juu ya adui zao.+
28 Basi wakaja Yerusalemu wakiwa na vinanda+ na vinubi+ na tarumbeta,+ kwenye nyumba ya Yehova.+
29 Na hofu+ ya Mungu ikawa juu ya falme zote za nchi waliposikia kwamba Yehova amepiga vita juu ya adui za Israeli.+
30 Kwa hiyo ufalme wa Yehoshafati haukuwa na usumbufu wowote, na Mungu wake akaendelea kumpa pumziko kuzunguka pande zote.+
31 Na Yehoshafati+ akaendelea kutawala juu ya Yuda. Alipoanza kutawala alikuwa na umri wa miaka 35, naye akatawala miaka 25 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Azuba+ binti ya Shilhi.
32 Naye akaendelea kutembea katika njia ya Asa+ baba yake, naye hakugeuka kando kutoka katika njia hiyo, kwa kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+
33 Ila tu mahali pa juu+ hapakuondolewa; na watu walikuwa bado hawajatayarisha moyo wao kwa ajili ya Mungu wa mababu zao.+
34 Na mambo mengine ya Yehoshafati, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa kati ya maneno ya Yehu+ mwana wa Hanani,+ yaliyoingizwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli.
35 Na baada ya hayo Yehoshafati mfalme wa Yuda akawa na ushirika na Ahazia+ mfalme wa Israeli, aliyetenda kwa uovu.+
36 Kwa hiyo akamfanya kuwa mshirika pamoja naye katika ujenzi wa meli za kwenda Tarshishi+ nao wakajenga meli kule Esion-geberi.+
37 Hata hivyo, Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii juu ya Yehoshafati, akisema: “Kwa sababu umefanya ushirika na Ahazia,+ hakika Yehova atazivunja kazi zako.”+ Basi zile meli zikavunjwa,+ nazo hazikuwa na nguvu za kwenda Tarshishi.+