2 Mambo ya Nyakati 2:1-18

2  Basi Sulemani akatoa amri kwamba nyumba+ ijengwe kwa ajili ya jina la Yehova+ na nyumba kwa ajili ya ufalme wake.+  Na Sulemani akahesabu watu 70,000 wawe wabeba-mizigo na 80,000 wawe wachongaji wa mawe mlimani,+ na 3,600 wawe waangalizi juu yao.+  Tena Sulemani akatuma watu kwa Hiramu+ mfalme wa Tiro, akisema: “Kama ulivyomtendea Daudi+ baba yangu, ulivyokuwa ukimletea mierezi ili ajijengee nyumba ya kukaa,—  tazama, ninajenga+ nyumba kwa ajili ya jina+ la Yehova Mungu wangu, ili niitakase+ kwake, ili kufukiza mbele zake uvumba uliotiwa manukato,+ pamoja na mkate+ wa tabaka wa daima na matoleo ya kuteketezwa wakati wa asubuhi na jioni,+ wakati wa sabato+ na wakati wa miezi mipya+ na kwenye majira ya sherehe+ ya Yehova Mungu wetu. Hayo yatakuwa juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo.+  Na nyumba nitakayoijenga itakuwa kuu,+ kwa maana Mungu wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.+  Na ni nani angeweza kuwa na nguvu za kumjengea nyumba?+ Kwa maana mbingu na mbingu za mbingu hazimtoshi,+ na mimi ni nani+ kwamba nimjengee nyumba isipokuwa tu iwe ya kufukizia moshi wa uvumba mbele zake?+  Na sasa niletee mwanamume mwenye ujuzi ili afanye kazi kwa kutumia dhahabu na fedha na shaba+ na chuma na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na uzi mwekundu na wa bluu, na anayejua jinsi ya kuchonga michoro, pamoja na wale walio na ustadi ambao wako pamoja nami katika Yuda na Yerusalemu, ambao Daudi baba yangu amewatayarisha.+  Nawe uniletee mierezi,+ miberoshi+ na misandali+ kutoka Lebanoni,+ kwa maana mimi najua vema kwamba watumishi wako wana uzoefu wa kukata miti ya Lebanoni,+ (na, tazama, watumishi wangu wako pamoja na watumishi wako,)  ili kunitayarishia miti kwa hesabu kubwa, kwa maana ile nyumba nitakayoijenga itakuwa kuu, ndiyo, kuu ajabu. 10  Na, tazama! kwa wakusanyaji wa mbao, wakataji wa miti, ninatoa chakula kwa watumishi wako, kori 20,000 za ngano,+ na kori 20,000 za shayiri, na bathi 20,000 za divai,+ na bathi 20,000 za mafuta.” 11  Ndipo Hiramu mfalme wa Tiro+ akatoa neno katika maandishi, akalituma kwa Sulemani: “Kwa sababu Yehova aliwapenda+ watu wake, amekufanya wewe kuwa mfalme juu yao.”+ 12  Na Hiramu akaendelea kusema: “Abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ aliyezifanya mbingu na dunia,+ kwa sababu amempa Mfalme Daudi mwana mwenye hekima, mwenye uzoefu katika busara na uelewaji,+ atakayejenga nyumba kwa ajili ya Yehova na nyumba kwa ajili ya ufalme wake.+ 13  Na sasa namtuma mtu mwenye ustadi, mwenye uzoefu katika uelewaji, Hiram-abi,+ 14  mwana wa mwanamke wa wana wa Dani lakini ambaye baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mwenye uzoefu, afanye mapambo ya dhahabu na fedha, shaba,+ chuma, mawe+ na miti, sufu iliyotiwa rangi ya zambarau,+ uzi wa bluu+ na kitambaa laini+ na uzi mwekundu+ na kuchonga kila namna ya michoro+ na kubuni kila namna ya kitu+ atakachoweza kupewa pamoja na watu wako wenye ustadi na watu wenye ustadi wa bwana wangu Daudi baba yako. 15  Na sasa ile ngano na shayiri, mafuta na divai ambavyo bwana wangu ameahidi, na avilete kwa watumishi wake.+ 16  Nasi tutakata miti+ kutoka Lebanoni kulingana na mahitaji yako yote,+ nasi tutakuletea kama vyelezo kupitia baharini+ mpaka Yopa,+ nawe utaichukua na kuipeleka Yerusalemu.” 17  Ndipo Sulemani akawahesabu watu wote waliokuwa wakaaji wageni, waliokuwa katika nchi ya Israeli,+ baada ya ile hesabu ya watu ambayo Daudi alikuwa amechukua;+ kukapatikana watu 153,600. 18  Kwa hiyo akawafanya 70,000 kati yao wawe wabeba-mizigo+ na 80,000 wawe wachongaji+ wa mawe mlimani na waangalizi 3,600 wa kuwafanya watu watumikie.+

Maelezo ya Chini