2 Mambo ya Nyakati 19:1-11

19  Kisha Yehoshafati mfalme wa Yuda akarudi kwa amani+ nyumbani kwake Yerusalemu.  Sasa Yehu+ mwana wa Hanani+ mwonaji+ akaenda mbele yake na kumwambia Mfalme Yehoshafati: “Je, waovu wanapaswa kupewa msaada,+ na je, unapaswa kuwapenda+ wale wanaomchukia+ Yehova? Kwa sababu hiyo kuna ghadhabu+ juu yako inayotoka mbele za uso wa Yehova.  Hata hivyo, kuna mambo mema+ ambayo yameonekana kwako, kwa sababu umeiondoa miti mitakatifu katika nchi+ nawe umetayarisha moyo wako kumtafuta Mungu wa kweli.”+  Na Yehoshafati akaendelea kukaa Yerusalemu; naye akaanza kutoka tena na kwenda katikati ya watu kutoka Beer-sheba+ mpaka eneo lenye milima la Efraimu,+ ili kuwarudisha kwa Yehova Mungu wa mababu zao.+  Naye akaweka waamuzi katika nchi yote katika majiji yote yenye ngome ya Yuda, jiji baada ya jiji.+  Naye akawaambia wale waamuzi: “Oneni mnalofanya,+ kwa sababu hamhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Yehova;+ naye yupo pamoja nanyi katika jambo la hukumu.+  Na sasa hofu+ ya Yehova na iwe juu yenu.+ Iweni waangalifu na mtende,+ kwa maana hakuna ukosefu wowote wa uadilifu+ wala ubaguzi+ wala kuchukua rushwa kwa upande wa Yehova Mungu wetu.”+  Na katika Yerusalemu pia Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi+ na makuhani+ na baadhi ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za Israeli kwa ajili ya uamuzi+ wa Yehova na kwa ajili ya kesi+ za wakaaji wa Yerusalemu.  Tena akaweka amri juu yao, akisema: “Hivi ndivyo mnavyopaswa kufanya katika kumwogopa+ Yehova kwa uaminifu na kwa moyo kamili. 10  Na kuhusu kila kesi itakayokuja kwenu ya ndugu zenu wanaokaa katika majiji yao, inayohusu kumwaga damu,+ inayohusu sheria+ na amri+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu,+ lazima mwaonye kwamba wasimkosee Yehova ili ghadhabu+ isije juu yenu na juu ya ndugu zenu. Hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya ili msipate hatia. 11  Na, tazama, yupo Amaria mkuu wa makuhani aliye juu yenu kwa ajili ya kila jambo la Yehova;+ na Zebadia mwana wa Ishmaeli kiongozi wa nyumba ya Yuda kwa ajili ya kila jambo la mfalme; nanyi mna Walawi wakiwa maofisa kwa ajili yenu. Iweni na nguvu,+ mtende, na Yehova+ awe pamoja na mambo yaliyo mema.”+

Maelezo ya Chini