2 Mambo ya Nyakati 18:1-34
18 Na Yehoshafati akawa na utajiri na utukufu kwa wingi;+ lakini akafanya mapatano ya ndoa+ pamoja na Ahabu.+
2 Basi miaka fulani baadaye akashuka kwa Ahabu huko Samaria;+ na Ahabu akamchinjia yeye na watu waliokuwa pamoja naye kondoo+ na ng’ombe kwa wingi. Naye akaanza kumshawishi+ wapande kupigana na Ramothi-gileadi.+
3 Na Ahabu mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Je, utaenda pamoja nami kule Ramothi-gileadi?”+ Ndipo akamwambia: “Mimi ni sawa na wewe, na watu wangu ni kama watu wako na tu pamoja nawe katika vita.”+
4 Hata hivyo, Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli: “Tafadhali, kwanza kabisa uliza+ upate neno la Yehova.”
5 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii+ pamoja, watu mia nne, akawaambia: “Je, twende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?”+ Nao wakaanza kusema: “Panda uende, na Mungu wa kweli atalitia jiji hilo mkononi mwa mfalme.”
6 Lakini Yehoshafati akasema: “Je, hayupo hapa tena nabii wa Yehova?+ Basi na tuulize kupitia yeye.”+
7 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati:+ “Bado kuna mtu mmoja+ ambaye tunaweza kumuuliza Yehova kupitia yeye, lakini hakika mimi ninamchukia,+ kwa maana katika siku zake zote yeye hatoi unabii wa mema kunihusu mimi, ila wa ubaya.+ Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.”+ Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme asiseme jambo kama hilo.”+
8 Basi mfalme wa Israeli akamwita ofisa wa makao ya mfalme+ na kusema: “Mlete haraka Mikaya mwana wa Imla.”+
9 Sasa mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja juu ya kiti chake cha ufalme, wakiwa wamevaa mavazi ya kifalme,+ nao walikuwa wameketi katika uwanja wa kupuria kwenye mwingilio wa lango la Samaria; na manabii wote walikuwa wakitenda kama manabii mbele yao.+
10 Ndipo Sedekia mwana wa Kenaana akajitengenezea pembe+ za chuma na kusema: “Yehova amesema hivi,+ ‘Kwa kutumia hizi utawasukuma Wasiria mpaka uwaangamize.’”+
11 Na wale manabii wengine wote walikuwa wakitoa unabii kama huo, wakisema: “Panda uende Ramothi-gileadi, upate mafanikio,+ na Yehova hakika atalitia jiji lile mkononi mwa mfalme.”+
12 Na yule mjumbe aliyeenda kumwita Mikaya akamwambia, akisema: “Tazama! Maneno ya manabii kwa kauli moja ni mema kwa mfalme; tafadhali, neno lako na liwe kama la mmoja wao,+ nawe useme mema.”+
13 Lakini Mikaya akasema: “Kama Yehova anavyoishi,+ lile ambalo Mungu wangu atasema, hilo ndilo nitakalosema.”+
14 Ndipo akaingia kwa mfalme, naye mfalme akamwambia: “Mikaya, je, twende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?” Mara moja akasema: “Panda uende na kufanikiwa; nao watatiwa mkononi mwenu.”+
15 Kwa hiyo mfalme akamwambia: “Ninakuapisha mara ngapi+ kwamba usiniambie jambo lolote ila kweli katika jina la Yehova?”+
16 Basi akasema: “Hakika ninawaona Israeli wote wametawanyika juu ya milima, kama kondoo wasio na mchungaji.+ Na Yehova akasema: ‘Hawa hawana mabwana.+ Kila mmoja na arudi kwa amani nyumbani kwake.’”+
17 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Je, sikukuambia, ‘Hatatoa unabii wa mambo mema kunihusu, ila tu mabaya’?”+
18 Naye akaendelea kusema: “Basi sikieni neno la Yehova:+ Hakika ninamwona Yehova ameketi juu ya kiti chake cha ufalme+ na jeshi+ lote la mbinguni limesimama upande wake wa kuume na wa kushoto.+
19 Na Yehova akasema, ‘Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli ili apande kwenda na kuanguka huko Ramothi-gileadi?’ Na kukawa na mazungumzo, huyu akisema hivi, na yule akisema vile.+
20 Mwishowe roho+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova, akasema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Ndipo Yehova akamwambia, ‘Kwa njia gani?’+
21 Naye akasema, ‘Nitaenda nami nitakuwa roho ya udanganyifu katika kinywa cha manabii wake wote.’+ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na tena utashinda.+ Nenda, ukafanye hivyo.’+
22 Na sasa, tazama, Yehova ametia roho ya udanganyifu katika kinywa cha hawa manabii wako wote;+ lakini Yehova mwenyewe ametangaza msiba juu yako.”+
23 Sasa Sedekia+ mwana wa Kenaana+ akakaribia, akampiga Mikaya+ kwenye shavu+ na kusema: “Ni katika njia gani hasa roho ya Yehova ilinipita mimi ikaenda kusema na wewe?”+
24 Kwa hiyo Mikaya akasema: “Tazama! Utaona ni njia gani siku ile+ utakapoingia katika chumba cha ndani kabisa ili ujifiche.”+
25 Ndipo mfalme wa Israeli akasema: “Mchukueni Mikaya, mmrudishe kwa Amoni mkuu wa jiji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.+
26 Nanyi mseme, ‘Mfalme amesema hivi: “Mtieni mtu huyu katika kizuizi,+ mkamlishe kwa posho iliyopunguzwa ya mkate+ na maji yaliyopunguzwa mpaka nitakaporudi kwa amani.”’”+
27 Basi Mikaya akasema: “Ukirudi kwa amani kwa vyovyote, Yehova hakusema nami.” Naye akaongezea:+ “Sikieni, enyi watu wote.”+
28 Na mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakapanda kwenda mpaka Ramothi-gileadi.+
29 Sasa mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Mimi nitajibadili sura+ na kuingia vitani, lakini wewe vaa mavazi yako.”+ Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadili sura, kisha wakaingia vitani.+
30 Naye mfalme wa Siria alikuwa amewaamuru wale wakuu wa magari yake, akisema: “Msipigane na mdogo wala na mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.”+
31 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipomwona Yehoshafati, wakaambiana: “Ndiye mfalme wa Israeli.”+ Basi wakageuka juu yake kupigana; na Yehoshafati akaanza kulia apewe msaada,+ na Yehova akamsaidia,+ na Mungu akawashawishi mara moja waondoke kwake.+
32 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipoona kwamba yeye hakuwa mfalme wa Israeli, mara moja wakaacha kumfuata.+
33 Na palikuwa na mtu aliyepinda upinde bila kujua, lakini akampiga+ mfalme wa Israeli katikati ya viungio na vazi la chuma, naye akamwambia mwendesha-gari:+ “Geuza mkono wako, uniondoe katika kambi, kwa sababu nimeumizwa vibaya.”+
34 Na pigano likazidi kuwa kali siku hiyo, na ikawa lazima kumweka mfalme wa Israeli akiwa amesimama katika gari akiwaelekea Wasiria mpaka jioni; na mwishowe akafa wakati wa kutua kwa jua.+