2 Mambo ya Nyakati 16:1-14

16  Katika mwaka wa 36 wa utawala wa Asa, Baasha+ mfalme wa Israeli alikuja kupigana na Yuda na kuanza kujenga Rama,+ ili asimruhusu mtu yeyote kutoka nje wala kuingia ndani kwa Asa mfalme wa Yuda.+  Sasa Asa akatoa fedha na dhahabu katika hazina za nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme,+ akazipeleka kwa Ben-hadadi+ mfalme wa Siria,+ aliyekuwa akikaa Damasko,+ akisema:  “Kuna agano kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, ninakuletea fedha na dhahabu. Nenda, vunja agano lako na Baasha+ mfalme wa Israeli, ili aondoke kwangu.”+  Basi Ben-hadadi akamsikiliza Mfalme Asa, akatuma wakuu wake wa majeshi kushambulia majiji ya Israeli, hivi kwamba wakapiga Iyoni+ na Dani+ na Abel-maimu+ na mahali pote penye maghala+ pa majiji ya Naftali.+  Na ikawa kwamba mara tu Baasha aliposikia habari hizo, mara moja akaacha kujenga Rama na kuikomesha kazi yake.+  Naye Asa mfalme akawachukua Yuda wote,+ nao wakachukua mawe ya Rama+ na miti yake ambayo Baasha alitumia kujenga,+ naye kwa vitu hivyo akaanza kujenga Geba+ na Mispa.+  Na wakati huo Hanani+ mwonaji akamjia Asa mfalme wa Yuda, kisha akamwambia: “Kwa sababu ulimwegemea mfalme wa Siria+ wala hukumwegemea Yehova Mungu wako,+ kwa sababu hiyo jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mkononi mwako.  Je, Waethiopia+ na Walibya+ hawakuwa jeshi kubwa sana kwa wingi, kwa magari na kwa wapanda-farasi;+ na kwa sababu ulimwegemea Yehova, je, hakuwatia mkononi mwako?+  Kwa maana, kwa habari ya Yehova, macho+ yake yanaenda huku na huku duniani+ kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo+ wao ni mkamilifu kumwelekea yeye. Umetenda kwa upumbavu+ kwa habari hii, kwa maana tangu sasa na kuendelea kutakuwa na vita juu yako.”+ 10  Hata hivyo, Asa akaudhika kwa sababu ya yule mwonaji, akamtia katika nyumba ya mikatale,+ kwa sababu alimwonea ghadhabu juu ya jambo hilo.+ Na Asa akaanza kuwakandamiza+ baadhi ya watu wakati huohuo. 11  Na, tazama! mambo ya Asa, ya kwanza na ya mwisho, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli. 12  Na Asa, katika mwaka wa 39 wa utawala wake, akapata ugonjwa katika miguu yake mpaka akawa mgonjwa sana;+ na hata katika ugonjwa wake hakumtafuta Yehova+ bali waponyaji.+ 13  Mwishowe Asa akalala pamoja na mababu zake,+ akafa katika mwaka wa 41 wa utawala wake. 14  Kwa hiyo wakamzika katika kaburi lake lenye fahari+ alilokuwa amejichimbia katika Jiji la Daudi;+ nao wakamlaza katika kitanda kilichojazwa mafuta ya zeri+ na aina mbalimbali za marhamu+ iliyochanganywa katika marhamu ya aina ya pekee.+ Tena wakamfanyia mfukizo wa mazishi+ ulio mkubwa isivyo kawaida.

Maelezo ya Chini