2 Mambo ya Nyakati 14:1-15
14 Mwishowe Abiya akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika katika Jiji la Daudi;+ na Asa+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. Katika siku zake nchi haikuwa na usumbufu+ kwa miaka kumi.
2 Na Asa akafanya yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake.
3 Basi akaondoa madhabahu za kigeni+ na mahali pa juu,+ akazivunja nguzo takatifu+ na kuikata miti mitakatifu.+
4 Tena akawaambia Yuda wamtafute+ Yehova Mungu wa mababu zao na kutenda sheria+ na amri.+
5 Kwa hiyo akaondoa katika majiji yote ya Yuda mahali pa juu na vinara vya uvumba;+ na ufalme ukaendelea bila usumbufu+ mbele yake.
6 Naye akajenga majiji yenye ngome katika Yuda,+ kwa maana nchi haikuwa na usumbufu; na hapakuwa na vita juu yake wakati wa miaka hiyo, kwa maana Yehova alimpa pumziko.+
7 Basi akawaambia Yuda: “Acheni tujenge majiji haya na tujenge kuta+ za kuzunguka na minara,+ milango yenye pande mbili na mapingo.+ Nchi bado inapatikana kwa ajili yetu, kwa sababu tumemtafuta Yehova Mungu wetu.+ Tumemtafuta, naye anatupa pumziko kuzunguka pande zote.”+ Nao wakajenga na kufanikiwa.+
8 Na Asa akawa na jeshi lenye kuchukua ngao kubwa+ na mkuki,+ watu 300,000 kutoka Yuda.+ Na kutoka Benyamini wale wanaochukua ngao ndogo na kupinda upinde+ walikuwa 280,000.+ Hao wote walikuwa mashujaa, wanaume wenye nguvu.
9 Baadaye Zera Mwethiopia+ akaenda kupigana nao akiwa na jeshi la watu milioni moja+ na magari mia tatu, akaja mpaka Maresha.+
10 Ndipo Asa akatoka kwenda juu yake, nao wakajipanga kivita katika bonde la Sefatha kule Maresha.
11 Naye Asa akaanza kumwita Yehova Mungu+ wake, na kusema: “Ee Yehova, kwa habari ya kusaidia, si kitu kwako kama kuna wengi au wale wasio na nguvu.+ Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana sisi tunakuegemea wewe,+ nasi kwa jina lako+ tumekuja kupigana na umati huu. Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu.+ Usiache mwanadamu anayeweza kufa apate nguvu juu yako.”+
12 Ndipo Yehova akawashinda+ Waethiopia mbele ya Asa na mbele ya Yuda, na Waethiopia wakakimbia.
13 Na Asa na watu waliokuwa pamoja naye wakaendelea kuwafuatilia mpaka Gerari,+ na walio wa Waethiopia wakaendelea kuanguka mpaka wakati ambapo hapakuwa na yeyote aliye hai kati yao; kwa maana walivunjwa vipande-vipande mbele za Yehova+ na mbele ya jeshi lake.+ Baadaye wakachukua kiasi kikubwa sana cha nyara.+
14 Tena wakayapiga majiji yote pande zote kuzunguka Gerari, kwa maana hofu+ ya Yehova ilikuwa imekuja juu yao; nao wakayapora majiji yote, kwa maana kulikuwa na vitu vingi vya kupora katika majiji hayo.+
15 Na hata wakayapiga mahema+ yenye mifugo hivi kwamba wakateka+ kwa wingi sana mifugo na ngamia,+ kisha wakarudi Yerusalemu.