2 Mambo ya Nyakati 12:1-16
12 Na ikawa kwamba mara tu ufalme wa Rehoboamu ulipofanywa imara+ na mara tu alipokuwa na nguvu, akaiacha sheria ya Yehova,+ na pia Israeli+ wote pamoja naye.
2 Na ikawa kwamba katika mwaka wa tano wa Mfalme Rehoboamu,+ Shishaki+ mfalme wa Misri akaja kushambulia Yerusalemu, (kwa maana walikuwa wamejiendesha kwa ukosefu wa uaminifu kwa Yehova,)+
3 akiwa na magari+ 1,200 na wapanda-farasi 60,000; na hawakuwa na hesabu+ wale watu waliotoka Misri pamoja naye —Walibya,+ Wasukii na Waethiopia.+
4 Naye akayateka majiji yenye ngome yaliyokuwa ya Yuda,+ na mwishowe akaja mpaka Yerusalemu.+
5 Sasa Shemaya+ nabii akamjia Rehoboamu na wakuu wa Yuda waliokuwa wamekusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, naye akawaambia: “Yehova amesema hivi, ‘Ninyi mmeniacha mimi,+ nami pia nimewaacha ninyi+ mkononi mwa Shishaki.’”
6 Ndipo wakuu wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza+ na kusema: “Yehova ni mwadilifu.”+
7 Na Yehova alipoona+ kwamba wamejinyenyekeza, neno la Yehova likamjia Shemaya,+ na kusema: “Wamejinyenyekeza.+ Sitawaharibu, na baada ya kitambo kidogo nitawafanya waponyoke, na ghadhabu yangu haitamwagika juu ya Yerusalemu kwa mkono wa Shishaki.+
8 Lakini wao watakuwa watumishi wake,+ ili wajue tofauti kati ya utumishi+ wangu na utumishi kwa falme za nchi.”+
9 Basi Shishaki+ mfalme wa Misri akapanda kushambulia Yerusalemu, akachukua hazina za nyumba ya Yehova+ na hazina za nyumba ya mfalme.+ Akachukua kila kitu; kwa hiyo akazichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+
10 Basi Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake, akaziweka chini ya wakuu wa wakimbiaji,+ walinzi+ wa mlango wa nyumba ya mfalme.+
11 Na ikawa ikitukia kwamba kila mara mfalme akija katika nyumba ya Yehova, wakimbiaji waliingia na kuzichukua na kuzirudisha katika chumba cha walinzi cha wakimbiaji.+
12 Na kwa sababu alijinyenyekeza, hasira ya Yehova ikageuka,+ ikaondoka juu yake, naye hakufikiria kuwaharibu kabisa.+ Na zaidi ya hayo, kulikuwa na mambo mema katika Yuda.+
13 Na Mfalme Rehoboamu akaendelea kuimarisha cheo chake katika Yerusalemu na kuendelea kutawala; kwa maana Rehoboamu+ alikuwa na umri wa miaka 41 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 17 katika Yerusalemu, jiji+ ambalo Yehova alichagua kutoka katika makabila yote ya Israeli ili kuweka jina lake humo.+ Na jina la mama yake lilikuwa Naama+ Mwamoni.+
14 Lakini yeye alifanya yaliyokuwa mabaya,+ kwa maana hakuwa ameufanya imara moyo wake ili kumtafuta Yehova.+
15 Na mambo ya Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho,+ je, hayakuandikwa kati ya maneno ya Shemaya+ nabii na Ido+ mwonaji kulingana na maandikisho ya kiukoo? Na kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu+ na Yeroboamu+ wakati wote.
16 Mwishowe Rehoboamu akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika Jiji la Daudi;+ na Abiya+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.