2 Mambo ya Nyakati 11:1-23
11 Rehoboamu alipofika Yerusalemu,+ mara moja akaikutanisha nyumba ya Yuda na Benyamini,+ wanaume bora, watu hodari wa vita,+ watu 180,000, wapigane na Israeli ili kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu.
2 Ndipo neno la Yehova likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli, na kusema:
3 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda+ na Israeli wote katika Yuda na Benyamini, ukisema,
4 ‘Yehova amesema hivi: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu.+ Mrudi kila mmoja nyumbani kwake, kwa maana jambo hili limetokea kwa mwongozo wangu.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova, wakarudi, ili wasiende kupigana na Yeroboamu.+
5 Na Rehoboamu akaendelea kukaa Yerusalemu, akajenga majiji yenye ngome katika Yuda.
6 Basi akajenga upya Bethlehemu+ na Etamu+ na Tekoa,+
7 na Beth-suri+ na Soko+ na Adulamu,+
8 na Gathi+ na Maresha+ na Zifu,+
9 na Adoraimu na Lakishi+ na Azeka,+
10 na Sora+ na Aiyaloni+ na Hebroni,+ majiji yenye ngome, yaliyokuwa katika Yuda na Benyamini.
11 Zaidi ya hayo, akaimarisha mahali penye ngome+ na kuweka viongozi+ ndani yake na akiba za chakula na mafuta na divai,
12 na katika majiji yote mbalimbali akaweka ngao+ kubwa na mikuki;+ naye akaendelea kuyaimarisha kwa kiwango kikubwa sana. Na watu wa Yuda na Benyamini wakaendelea kuwa wake.
13 Na makuhani na Walawi waliokuwa katika Israeli yote wakasimama upande wake kutoka katika maeneo yao yote.
14 Kwa maana Walawi waliviacha viwanja vyao vya malisho+ na miliki+ yao kisha wakaja Yuda na Yerusalemu,+ kwa sababu Yeroboamu+ na wanawe walikuwa wamewaondoa+ wasiwe makuhani kwa Yehova.
15 Naye akajiwekea mwenyewe katika cheo makuhani wa mahali pa juu+ na wa roho waovu wenye umbo la mbuzi+ na wa wale ndama aliokuwa ametengeneza.+
16 Na wale waliowafuata kutoka katika makabila yote ya Israeli, ambao walikuwa wakitoa moyo wao kumtafuta Yehova Mungu wa Israeli, wakaja Yerusalemu+ kumtolea dhabihu+ Yehova Mungu wa mababu zao.
17 Nao wakaendelea kuutia nguvu ufalme wa Yuda+ na kumthibitisha Rehoboamu mwana wa Sulemani kwa miaka mitatu, kwa maana walitembea katika njia ya Daudi na Sulemani kwa miaka mitatu.+
18 Ndipo Rehoboamu akamchukua Mahalathi binti ya Yerimothi mwana wa Daudi awe mke wake, na ya Abihaili binti ya Eliabu+ mwana wa Yese.
19 Baada ya muda akamzalia wana, Yeushi na Shemaria na Zahamu.
20 Na baada yake akamchukua Maaka+ mjukuu wa Absalomu.+ Baada ya muda akamzalia Abiya+ na Atai na Ziza na Shelomithi.
21 Na Rehoboamu alimpenda zaidi Maaka mjukuu wa Absalomu kuliko wale wake+ zake wengine wote na masuria wake; kwa maana alikuwa amechukua wake 18, pia masuria 60, hivi kwamba akawa na wana 28 na binti 60.
22 Kwa hiyo Rehoboamu akamweka Abiya mwana wa Maaka katika cheo awe kichwa, awe kiongozi kati ya ndugu zake, kwa maana alifikiria kumfanya kuwa mfalme.
23 Hata hivyo, akatenda kwa uelewaji+ na kuwagawanya baadhi ya wanawe wote kwenye nchi zote za Yuda na Benyamini,+ kwenye majiji yote yenye ngome,+ akawapa chakula kwa wingi+ na kuwachukulia wake wengi.+