2 Mambo ya Nyakati 1:1-17

1  Naye Sulemani mwana wa Daudi akaendelea kupata nguvu katika ufalme wake,+ na Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye,+ akaendelea kumfanya kuwa mkuu zaidi.+  Na Sulemani akasema na Israeli wote, kwa wakuu wa maelfu+ na wa mamia+ na kwa waamuzi+ na wakuu wote wa Israeli,+ vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba.+  Kisha Sulemani na kutaniko lote pamoja naye wakaenda mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni;+ kwa maana hapo ndipo lilipokuwa lile hema la mkutano+ la Mungu wa kweli, ambalo Musa mtumishi+ wa Yehova alitengeneza nyikani.  Hata hivyo, Daudi alikuwa amelileta sanduku+ la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu+ mpaka mahali ambapo Daudi alikuwa amelitayarishia,+ kwa maana alikuwa amelisimamishia hema katika Yerusalemu.+  Na ile madhabahu ya shaba+ ambayo Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru+ alikuwa ametengeneza ilikuwa imewekwa mbele ya maskani ya Yehova; na Sulemani na kutaniko wakatoa maombi yao mbele yake kama kawaida.  Kisha Sulemani akafanya matoleo hapo mbele za Yehova juu ya ile madhabahu ya shaba ya hema la mkutano, naye akatoa juu yake matoleo elfu moja ya kuteketezwa.+  Usiku huo Mungu akamtokea Sulemani na kumwambia: “Omba! Nikupe nini?”+  Ndipo Sulemani akamwambia Mungu: “Wewe Ndiye uliyemwonyesha Daudi baba yangu+ fadhili kubwa zenye upendo na kunifanya niwe mfalme mahali pake.+  Sasa, Ee Yehova Mungu, acha ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie,+ kwa maana wewe mwenyewe umenifanya kuwa mfalme+ juu ya watu wengi sana kama chembe za mavumbi ya dunia.+ 10  Sasa unipe hekima na ujuzi+ ili nitoke mbele ya watu hawa na ili niingie ndani,+ kwa maana ni nani anayeweza kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?”+ 11  Ndipo Mungu akamwambia Sulemani: “Kwa sababu jambo hili liko moyoni+ mwako nawe hukuomba mali, utajiri wala heshima wala nafsi ya wale wanaokuchukia, wala hata hukuomba wingi wa siku,+ bali unaomba hekima na ujuzi kwa ajili yako ili uwahukumu watu wangu ambao nimekufanya kuwa mfalme juu yao,+ 12  unapewa hekima na ujuzi;+ pia nitakupa mali na utajiri na heshima ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekutangulia amepata kuwa navyo,+ wala baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”+ 13  Basi Sulemani akatoka pale mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni,+ kutoka mbele ya hema la mkutano,+ akaja Yerusalemu, akaendelea kutawala juu ya Israeli.+ 14  Na Sulemani akaendelea kukusanya magari na farasi wa vita hivi kwamba akawa na magari elfu moja na mia nne na farasi wa vita kumi na mbili elfu,+ akawaweka katika majiji ya magari+ na karibu na mfalme katika Yerusalemu. 15  Na mfalme akafanya fedha na dhahabu iliyomo Yerusalemu kuwa kama mawe;+ naye akafanya mierezi iwe kama mikuyu+ iliyoko Shefela+ kwa wingi. 16  Na farasi wa Sulemani walisafirishwa kutoka Misri,+ na wanabiashara wa mfalme wakawa wakichukua kundi la farasi kwa bei fulani.+ 17  Nao wakawa wakipandisha na kusafirisha kwa ukawaida gari kutoka Misri kwa vipande 600 vya fedha na farasi kwa vipande 150; na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wafalme wote wa Wahiti na wafalme wa Siria.+ Walikuwa wakisafirisha vitu kupitia hao.

Maelezo ya Chini