1 Mambo ya Nyakati 2:1-55

2  Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli:+ Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi+ na Yuda,+ Isakari+ na Zabuloni,+  Dani,+ Yosefu+ na Benyamini,+ Naftali,+ Gadi+ na Asheri.+  Wana wa Yuda walikuwa Eri+ na Onani+ na Shela.+ Binti ya Shua, mwanamke Mkanaani, alimzalia wana hao watatu. Na Eri mzaliwa wa kwanza wa Yuda akawa mbaya machoni pa Yehova, hivi kwamba yeye akamuua.+  Na Tamari+ binti-mkwe wake ndiye aliyemzalia Perezi+ na Zera. Wana wote wa Yuda walikuwa watano.  Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+  Na wana wa Zera+ walikuwa Zimri na Ethani na Hemani na Kalkoli na Dara.+ Jumla yao walikuwa watano.  Na wana wa Karmi+ walikuwa Akari aliyeleta taabu juu ya Israeli,+ ambaye alitenda tendo la kukosa uaminifu kwa habari ya kile kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa.+  Na wana wa Ethani+ walikuwa Azaria.  Na wana wa Hezroni+ aliozaa walikuwa Yerahmeeli+ na Ramu+ na Kelubai. 10  Ramu naye akamzaa Aminadabu.+ Naye Aminadabu akamzaa Nashoni+ mkuu wa wana wa Yuda. 11  Naye Nashoni akamzaa Salma.+ Naye Salma akamzaa Boazi.+ 12  Naye Boazi akamzaa Obedi.+ Naye Obedi akamzaa Yese.+ 13  Naye Yese akamzaa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu,+ na Abinadabu+ wa pili, na Shimea+ wa tatu, 14  Nethaneli wa nne, Radai wa tano, 15  Ozemu wa sita, Daudi+ wa saba. 16  Na dada zao walikuwa Seruya na Abigaili;+ na wana wa Seruya walikuwa Abishai+ na Yoabu+ na Asaheli,+ watatu. 17  Abigaili naye alimzaa Amasa;+ na baba ya Amasa alikuwa Yetheri,+ Mwishmaeli. 18  Naye Kalebu mwana wa Hezroni,+ akazaa wana kupitia kwa Azuba mke wake na kupitia kwa Yeriothi; na hawa ndio waliokuwa wana wa mke wake: Yesheri na Shobabu na Ardoni. 19  Mwishowe Azuba akafa. Kwa hiyo Kalebu akamchukua Efrathi,+ ambaye baada ya muda alimzalia Huru.+ 20  Naye Huru akamzaa Uri.+ Naye Uri akamzaa Bezaleli.+ 21  Na baadaye Hezroni akalala na binti ya Makiri+ baba ya Gileadi.+ Naye alikuwa na umri wa miaka 60 alipomchukua binti huyo, lakini akamzalia Segubu. 22  Naye Segubu akamzaa Yairi,+ aliyekuja kuwa na majiji 23+ katika nchi ya Gileadi. 23  Baadaye Geshuri+ na Siria+ wakachukua Hawoth-yairi+ kutoka kwao, na Kenathi+ na miji yake ya kandokando, majiji 60. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Makiri baba ya Gileadi. 24  Na baada ya kifo cha Hezroni+ katika Kalebu-efratha, Abiya akiwa mke wa Hezroni, ndipo alipomzalia Ashuri baba ya Tekoa.+ 25  Na wana wa Yerahmeeli+ mzaliwa wa kwanza wa Hezroni walikuwa Ramu+ mzaliwa wa kwanza na Buna na Oreni na Ozemu, Ahiya. 26  Na Yerahmeeli akaja kuwa na mke mwingine, ambaye jina lake lilikuwa Atara. Yeye ndiye alikuwa mama ya Onamu. 27  Na wana wa Ramu+ mzaliwa wa kwanza wa Yerahmeeli walikuwa Maazi na Yamini na Ekeri. 28  Na wana wa Onamu+ walikuja kuwa Shamai na Yada. Na wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri. 29  Na jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, ambaye baada ya muda alimzalia Abani na Molidi. 30  Na wana wa Nadabu+ walikuwa Seledi na Apaimu. Lakini Seledi alikufa bila kuwa na wana. 31  Na wana wa Apaimu walikuwa Ishi. Na wana wa Ishi walikuwa Sheshani; na wana wa Sheshani,+ Alai. 32  Na wana wa Yada ndugu ya Shamai walikuwa Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alikufa bila kuwa na wana. 33  Na wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hao wakawa wana wa Yerahmeeli. 34  Na Sheshani+ hakuwa na wana wowote, ila mabinti. Sasa Sheshani alikuwa na mtumishi Mmisri+ ambaye jina lake lilikuwa Yarha. 35  Basi Sheshani akampa Yarha mtumishi wake binti yake awe mke wake, ambaye baada ya muda alimzalia Atai. 36  Naye Atai akamzaa Nathani. Naye Nathani akamzaa Zabadi.+ 37  Naye Zabadi akamzaa Eflali. Naye Eflali akamzaa Obedi. 38  Naye Obedi akamzaa Yehu. Naye Yehu akamzaa Azaria. 39  Naye Azaria akamzaa Helezi. Naye Helezi akamzaa Eleasa. 40  Naye Eleasa akamzaa Sismai. Naye Sismai akamzaa Shalumu. 41  Naye Shalumu akamzaa Yekamia. Naye Yekamia akamzaa Elishama. 42  Na wana wa Kalebu+ ndugu ya Yerahmeeli walikuwa Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa baba ya Zifu, na wana wa Maresha baba ya Hebroni. 43  Na wana wa Hebroni walikuwa Kora na Tapua na Rekemu na Shema. 44  Naye Shema akamzaa Rahamu baba ya Yorkeamu. Naye Rekemu akamzaa Shamai. 45  Na mwana wa Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa baba ya Beth-suri.+ 46  Na Efa suria wa Kalebu, yeye alimzaa Harani na Mosa na Gazezi. Harani naye akamzaa Gazezi. 47  Na wana wa Yahdai walikuwa Regemu na Yothamu na Geshani na Peleti na Efa na Shaafu. 48  Na Maaka, suria wa Kalebu, yeye alizaa Sheberi na Tirhana. 49  Baada ya muda akamzaa Shaafu baba ya Madmana,+ Sheva baba ya Makbena na baba ya Gibea.+ Na binti ya Kalebu+ alikuwa Aksa.+ 50  Hao wakawa wana wa Kalebu. Wana wa Huru+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha:+ Shobali+ baba ya Kiriath-yearimu,+ 51  Salma baba ya Bethlehemu,+ Harefu baba ya Beth-gaderi. 52  Na Shobali+ baba ya Kiriath-yearimu akaja kuwa na wana: Haroe, nusu ya Menuhothi. 53  Na familia za Kiriath-yearimu zilikuwa Waithri+ na Waputhu na Washumathi na Wamishra. Wasorathi+ na Waeshtaoli+ walitoka kwa hao. 54  Wana wa Salma walikuwa Bethlehemu+ na Wanetofa,+ Atroth-beth-yoabu na nusu ya Wamanahathi, Wazori. 55  Na familia za waandishi waliokaa katika Yabesi+ zilikuwa Watirathi, Washimea, Wasukathi. Hao walikuwa Wakeni+ waliotokana na Hamathi baba ya nyumba ya Rekabu.+

Maelezo ya Chini