Je, Biblia Ni Kitabu Chenye Rekodi ya Mawazo ya Mungu?
Jibu la Biblia
Waandikaji wengi wa Biblia wanasema kwamba Mungu aliwaongoza katika kuandika mambo waliyoandika. Ona mifano ifuatayo:
Mfalme Daudi: “Roho ya Yehova ndiyo iliyosema kupitia mimi, na neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.”—2 Samweli 23:1, 2.
Nabii Isaya: “Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, amesema hivi.”—Isaya 22:15.
Mtume Yohana: “Ufunuo kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa.”—Ufunuo 1:1.