Kwa Nini Watu Hufa?

Kwa Nini Watu Hufa?

Jibu la Biblia

 Ni jambo la kawaida kujiuliza kwa nini watu hufa, hasa mpendwa wetu wa karibu anapokufa. Biblia inasema: “Mchomo unaotokeza kifo ni dhambi.”​—1 Wakorintho 15:56.

Kwa nini watu wote wanatenda dhambi na kufa?

 Wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa, walipoteza uhai wao kwa sababu walitenda dhambi. (Mwanzo 3:17-19) Kifo kilikuwa matokeo ya uasi wao dhidi ya Mungu, kwa sababu yeye ndiye “chemchemi ya uzima.”​—Zaburi 36:9; Mwanzo 2:17.

  Adamu alipitisha matokeo ya dhambi kwa wazao wake wote. Biblia inasema: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Waroma 5:12) Wanadamu wote hufa kwa sababu wote wanatenda dhambi.​—Waroma 3:23.

Jinsi kifo kitakavyoondolewa

 Mungu anaahidi wakati ambapo “atameza kifo milele.” (Isaya 25:8) Ili kumaliza kifo, lazima aondoe dhambi, chanzo cha kifo. Mungu atatimiza hayo kupitia Yesu Kristo, “ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.”​—Yohana 1:29; 1 Yohana 1:7.