HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 1-10
Ili Tuwe na Amani na Yehova Lazima Tumbusu Mwana Wake, Yesu
Chuki dhidi ya Yehova na Yesu ilitabiriwa mapema
Ilitabiriwa kwamba mataifa yangekataa mamlaka ya Yesu bali yangesisitiza mamlaka ni yao
Unabii huo ulitimizwa Yesu alipokuwa duniani na unatimizwa kwa njia kubwa zaidi leo
Mtunga-zaburi anasema kwamba mataifa yanasema jambo la upuuzi, kumaanisha kwamba kusudi lao ni la bure na halitafanikiwa
Wale tu wanaomheshimu Mfalme mtiwa-mafuta wa Yehova ndio watakaopata uzima
Wote wanaompinga Mfalme wa Kimasihi wataangamizwa
Kwa kumbusu Mwana, au kuheshimu mamlaka ya Yesu, mtu anaweza kupata usalama na amani