HAZINA ZA NENO LA MUNGU | SEFANIA 1–HAGAI 2
Mtafute Yehova Kabla ya Siku Yake ya Hasira
Ili Yehova atufiche katika siku yake ya hasira, tunapaswa kufanya mengi zaidi ya kujiweka wakfu kwake. Tunapaswa kutii mwongozo ambao Sefania aliwapa Waisraeli.
Mtafuteni Yehova: Dumisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova kwa kushirikiana na tengenezo lake
Utafuteni uadilifu: Dumisha viwango vya uadilifu vya Yehova
Utafuteni upole: Jitiishe kwa Mungu ili kufanya mapenzi yake kwa unyenyekevu na ukubali nidhamu kutoka kwake
Ninaweza kumtafutaje Yehova, uadilifu, na upole kwa kiwango kikubwa zaidi?