Malaki 4:1-6
4 “Kwa maana, tazama! siku ile inakuja ambayo inawaka kama tanuru,+ na wote wenye kimbelembele na wote wanaotenda uovu watakuwa kama majani makavu.+ Na siku hiyo inayokuja itawateketeza,” Yehova wa majeshi amesema, “hivi kwamba haitawaachia wao mzizi wala tawi.+
2 Na kwenu ninyi mnaoliogopa jina langu, jua la uadilifu litaangaza,+ likiwa na kiponyaji katika mabawa yake;+ nanyi mtatoka nje na kuukanyaga udongo kama ndama waliononeshwa.”+
3 “Nanyi mtawakanyagia chini waovu, kwa maana watakuwa kama mavumbi chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayochukua hatua,”+ asema Yehova wa majeshi.
4 “Ikumbukeni sheria ya Musa mtumishi wangu niliyomwamuru katika Horebu kuhusu Israeli wote, hata masharti na maamuzi ya hukumu.+
5 “Tazama! Nawatumia ninyi nabii Eliya+ kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.+
6 Naye atageuza moyo wa akina baba urudi kwa wana, na moyo wa wana urudi kwa akina baba; ili nisije kuipiga dunia na kuiangamiza.”+