Isaya 23:1-18
23 Tangazo la Tiro:+ Pigeni mayowe, enyi meli za Tarshishi!+ kwa maana imeporwa isiwe bandari tena, isiwe mahali pa kuingia.+ Wamefunuliwa habari kutoka katika nchi ya Kitimu.+
2 Kaeni kimya, enyi wakaaji wa nchi ya pwani. Wanabiashara kutoka Sidoni,+ wale wanaovuka bahari—wamekujaza.
3 Na mbegu ya Shihori+ imekuwa juu ya maji mengi, mavuno ya Nile, mapato yake; nayo yakaja kuwa faida ya mataifa.+
4 Ona aibu, Ee Sidoni;+ Ee ngome ya bahari, kwa sababu bahari imesema: “Sijapata uchungu wa kuzaa, nami sijazaa, wala sijalea vijana, wala kulea mabikira.”+
5 Kama vile wakati wa ile habari juu ya Misri,+ ndivyo watu watakavyokuwa na maumivu makali wakati wa ile habari juu ya Tiro.+
6 Vukeni mpaka Tarshishi; pigeni mayowe, enyi wakaaji wa nchi ya pwani.
7 Je, hili ndilo jiji lenu lililokuwa na furaha tangu siku za kale, tangu nyakati zake za zamani? Miguu yake ilikuwa ikimpeleka mbali kukaa kama mgeni.
8 Ni nani ambaye ametoa shauri hili+ juu ya Tiro, mwenye kuvika watu mataji, ambaye wanabiashara wake walikuwa wakuu, ambaye wafanya-biashara wake walikuwa watu wenye vyeo wa dunia?+
9 Yehova wa majeshi mwenyewe ametoa shauri hili,+ kutia unajisi kiburi cha uzuri wote,+ kuwatendea kwa dharau watu wote wenye vyeo wa dunia.+
10 Vuka juu ya nchi yako kama Mto Nile, Ee binti Tarshishi.+ Hakuna tena kiwanda cha meli.+
11 Ameunyoosha mkono wake juu ya bahari; amezifadhaisha falme.+ Yehova mwenyewe ametoa amri juu ya Foinike, ya kuziangamiza ngome zake.+
12 Naye asema: “Usifurahi kamwe tena,+ ewe uliyekandamizwa, bikira binti Sidoni.+ Simama, vuka mpaka Kitimu.+ Hata huko hakutakuwa na utulivu kwako.”
13 Tazama! Nchi ya Wakaldayo.+ Hiki ndicho kikundi cha watu—Ashuru+ hakujionyesha kuwa hicho—walimweka awe msingi kwa ajili ya wakaaji wa jangwani.+ Wamesimamisha minara yao ya kuzingira;+ wameivua minara yake ya makao;+ mtu amemweka kuwa bomoko linaloharibika.+
14 Pigeni mayowe, enyi meli za Tarshishi, kwa maana ngome yenu imeporwa.+
15 Na itatukia katika siku hiyo kwamba Tiro lazima lisahauliwe kwa miaka 70,+ sawasawa na siku za mfalme mmoja. Mwishoni mwa ile miaka 70 itakuwa kwa Tiro kama katika wimbo wa kahaba:
16 “Chukua kinubi, lizunguke jiji, Ee kahaba uliyesahauliwa.+ Fanya kila unaloweza kupiga vinanda; fanya nyimbo zako ziwe nyingi, ili upate kukumbukwa.”
17 Na itatukia kwamba mwishoni mwa miaka 70 Yehova atakaza fikira zake juu ya Tiro, naye atarudia malipo+ yake na kufanya ukahaba na falme zote za dunia zilizo juu ya uso wa nchi.+
18 Na faida yake na malipo+ yake lazima viwe kitu kitakatifu kwa Yehova. Havitawekwa akiba, wala kurundikwa, kwa sababu malipo yake yatakuja kuwa ya wale wanaokaa mbele za Yehova,+ kwa ajili ya kula na kushiba na kwa ajili ya mavazi yenye fahari.+