Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu Yaridhishwa na Hatua ya Serikali ya Georgia Kukiri Kuwa na Hatia
Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu(ECHR) yaridhishwa na hatua ya Jamhuri ya Georgia kukiri kuwa ilikiuka haki za Mashahidi wa Yehova kumi.
Kazakhstan Imepatikana na Hatia ya Kumfunga Isivyo Haki Teymur Akhmedov
Kikundi cha Umoja wa Mataifa Kinachoshughulikia Vifungo Vilivyo Kinyume cha Sheria kimeeleza kwamba Kazakhstan ina hatia ya kumkamata na kumfungulia mashtaka isivyo haki Bw. Akhmedov kwa sababu ya kuwaeleza kwa amani watu wengine mambo anayoamini.
Ujerumani Imewapa Mashahidi wa Yehova Usajili wa Pekee wa Kisheria
Baada ya kuendesha kesi kwa miaka zaidi ya 26, Mashahidi wamepata usajili uleule wa kisheria ambao dini nyingine kubwa nchini zinapata.
Watu Wengi Watoa Maoni Kuhusu Kutambuliwa kwa Haki ya Kukataa Kujiunga na Jeshi kwa Sababu ya Dhamiri Nchini Korea Kusini
Hata ingawa hakuna uamuzi uliofanywa na mahakama au sheria mpya iliyotungwa, Korea Kusini imeboresha maoni yake kuhusu wale wanaokataa kujiunga na utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri.
Urusi Yaitangaza Biblia Kuwa na “Msimamo Mkali”
Mahakama ya Jiji la Vyborg iliitangaza Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya lugha ya Kirusi kuwa na ‘msimamo mkali,’ Biblia hiyo inachapishwa na Mashahidi wa Yehova katika lugha nyingi.
Programu Yenye Mafanikio ya Utumishi wa Badala wa Kiraia Nchini Taiwan
Taiwan yatoa utumishi wa badala wa kiraia kama nafasi ya wale wanaokataa kujiunga na utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri.
Maoni ya Mataifa Mbalimbali Kuhusu Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Urusi Dhidi ya Mashahidi wa Yehova
Mashirika mbalimbali ya kimataifa na maofisa mbalimbali wametoa maoni kuhusu uamuzi usio wa haki wa mahakama na serikali ya Urusi kushindwa kulinda uhuru wa ibada wa dini zenye waumini wachache.
Mahakama Kuu ya Urusi Imehalalisha Hukumu Yake ya Awali ya Kuwapiga Marufuku Mashahidi wa Yehova
Mahakama Kuu ya Urusi imekataa rufaa ya Mashahidi na kuthibitisha uamuzi wake wa Aprili 20. Mashahidi wa Yehova nchini Urusi watakata rufaa ili wapate haki katika ECHR na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu.