Maoni ya Wataalamu Kuhusu Haki ya Kukataa Utumishi wa Kijeshi kwa Sababu ya Dhamiri
Haki ya kukataa utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri ni haki ya msingi inayokubalika karibu katika kila nchi. Sikiliza uelewe kwa nini wataalamu wa haki za kibinadamu wanasema kwamba hivi karibuni suala hilo litatambulika ulimwenguni pote.
Uhuru wa Ibada Wakandamizwa Nchini Urusi
Kesi imefunguliwa dhidi ya Mashahidi wa Yehova kule Taganrog, Urusi. Jumba lao la Ufalme limechukuliwa pamoja na machapisho yao.
Raia wa Urusi Washtakiwa kwa Sababu ya Imani Yao
Kuhukumiwa kwa Mashahidi wa Yehova wanaokabili mashtaka ya uhalifu huko Taganrog kutahatarisha haki za msingi za raia wote wa Urusi.
Kuna Tumaini kwa Mashahidi wa Yehova Nchini Uzbekistan?
Inaonekana kwamba wenye mamlaka nchini Uzbekistan wameanza kuona umuhimu wa kuzingatia haki za kibinadamu. Mashahidi wa Yehova wanatarajia kwamba hali zitabadilika na makutaniko yote yatasajiliwa.
Uturuki Haitafuata Viwango vya Ulaya Kuhusu Kukataa Utumishi wa Kijeshi kwa Sababu ya Dhamiri
Kwa nini serikali hiyo imekataa kutambua haki ya wale wanaokataa utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri, haki ambayo ni ya msingi kwa kila mwanadamu?
Mahakama ya Rufani ya Urusi Yakataa Kupiga Marufuku JW.ORG
Mahakama ya Mkoa wa Tver nchini Urusi ilibatilisha uamuzi uliokuwa umetolewa na Mahakama ya Wilaya, uamuzi wa kupiga marufuku jw.org—tovuti rasmi ya Mashahidi wa Yehova.
Korea Kusini Yawatenganisha Waliofungwa kwa Sababu ya Dhamiri Kutoka kwa Wafungwa wa Uhalifu
Korea Kusini imewapa kitulizo mamia ya Mashahidi wa Yehova ambao wamefungwa gerezani kwa kukataa utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri.
Armenia Yaruhusu Wanaokataa Kujiunga na Jeshi kwa Sababu ya Dhamiri Wafanye Utumishi wa Badala wa Kiraia
Inaonekana Armenia imetambua haki za wale wanaokataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri. Mashahidi kadhaa wameruhusiwa kufanya utumishi wa badala wa kiraia.
Jamii ya Kimataifa Yalalamikia Ukosefu wa Haki wa Korea Kusini
Broshua mpya iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova inazungumzia kufungwa gerezani isivyo haki kwa mamia ya watu wanaokataa kufanya utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri.
Shirika la Umoja wa Mataifa Lasema Lazima Uturuki Iheshimu Dhamiri ya Raia Wake
Soma kuhusu uamuzi muhimu uliofanywa na Umoja wa Mataifa kwamba raia wa Uturuki wana haki ya kukataa utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri.
Uamuzi wa Mahakama, “Hatuishi Katika Mwaka wa 1937”
Jaji wa mahakama ya wilaya alifutilia mbali uamuzi wa mahakama ya chini.
Maamuzi ya Haki Yatolewa Nchini Ukrainia
Mahakama Kuu ya Ukrania ilizuia jaribio lisilo la haki la watu waliotaka kunyakua uwanja ambao ni mali halali ya Mashahidi wa Yehova