FEBRUARI 9, 2024 | HABARI ZIMEONGEZWA: DESEMBA 6, 2024
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI—DADA WAHUKUMIWA | Kukabiliana na Majaribu Huku Wakimtumaini Yehova
Desemba 6, 2024, Mahakama ya Jiji la Blagoveshchensk iliyo katika Eneo la Amur iliwahukumu Dada Kristina Golik, Dada Yekaterina Olshevskaya, Dada Mariya Myasnikova, na Dada Valentina Yermilova. Kristina na Valentina walihukumiwa kila mmoja kifungo cha miaka miwili na miezi sita na watafanya kazi ya kulazimishwa. Mariya na Yekaterina walihukumiwa kila mmoja kifungo cha miaka miwili na miezi miwili na watafanya kazi ya kulazimishwa. Wote wanne watakaa gerezani na watakuwa wakienda kufanya kazi walizopangiwa katika jamii.
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tunamshukuru Yehova kwa vielelezo ambavyo dada hawa wanatuwekea. Na tunajua kwamba Yehova ataendelea kuwatunza na kuwabariki.—Zaburi 27:3.
Mfuatano wa Matukio
Julai 20, 2018
Nyumba zilifanyiwa msako
Julai 22, 2021
Dada wote wanne walishtakiwa kuwa wahalifu
Julai 27, 2021
Kristina na Mariya waliwekewa vizuizi vya kusafiri
Agosti 3, 2021
Yekaterina aliwekewa vizuizi vya kusafiri
Agosti 4, 2021
Valentina aliwekewa vizuizi vya kusafiri
Mei 26, 2023
Kesi ya uhalifu ilianza

