Kiswahili
Vitabu vya Biblia Vyatolewa Katika Mwezi Julai 2025
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/702025091/univ/art/702025091_univ_sqr_xl.jpg

AGOSTI 13, 2025
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Vitabu vya Biblia Vyatolewa Katika Mwezi Julai 2025

Vitabu vya Biblia Vyatolewa Katika Mwezi Julai 2025

Kilari

Julai 4, 2025, Ndugu Delphin Kavusa, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa), alitangaza kutolewa kwa Biblia—Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kilari. Alitangaza pia kutolewa kwa vitabu vifuatavyo: Marko, Luka, Yohana, Matendo, Waroma, 1 Wakorintho, Wagalatia, na Wafilipi katika lugha hiyo. Vitabu hivyo tisa vya Biblia, vilitolewa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Brazzaville, katika Jamhuri ya Kongo. Watu 1,022 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja wao alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia—Habari Njema Kulingana na Mathayo. Vitabu vyote tisa vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Kuna watu milioni 1.5 hivi wanaozungumza Kilari katika Jamhuri ya Kongo. Mashahidi wa Yehova walianza kuchapisha machapisho yanayotegemea Biblia katika lugha hiyo mwaka wa 1996. Leo, kuna ndugu na dada 500 hivi wanaotumikia katika makutaniko saba ya Kilari kotekote nchini humo.

Kivalencia

Julai 4, 2025, Ndugu José García, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Hispania, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kivalencia. Tangazo hilo lilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa kwenye Jumba la Kusanyiko la Benidorm jijini Alicante. Watu 702 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana na wengine 250 waliunganishwa kupitia video mtandaoni. Wale waliohudhuria walipata nakala zilizochapishwa za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Biblia hiyo ilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Kuna watu milioni 2.5 wanaozungumza Kivalencia nchini Hispania, kutia ndani ndugu na dada zetu 760 wanaotumikia katika makutaniko 15 ya Kivalencia.

Kicinamwanga

Julai 11, 2025, Ndugu Kena Kunda, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Zambia, alitangaza kutolewa kwa Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kicinamwanga. Alitangaza pia kutolewa kwa vitabu vifuatavyo: Marko, Luka, na Yohana katika lugha hiyo. Vitabu hivyo vinne vya Biblia, vilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Isoka, Zambia. Watu 1,134 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja wao alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo. Vitabu vyote vinne vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa katika mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Isitoshe, rekodi za sauti za vitabu hivyo vinne zilipatikana pia.

Inakadiriwa kwamba kuna watu 140,000 wanaoishi nchini Zambia wanaozungumza Kicinamwanga. Leo, kuna ndugu na dada 3,000 hivi wanaotumikia katika makutaniko 52 ya Kicinamwanga kotekote nchini humo.

Kigalicia

Julai 11, 2025, Ndugu Andrew Weaver, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Hispania, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kigalicia. Tangazo hilo lilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Santiago de Compostela. Watu 878 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja wao alipata nakala iliyochapishwa ya toleo hilo. Pia, toleo hilo lilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Kuna watu milioni 3.4 hivi wanaozungumza Kigalicia ulimwenguni pote. Nchini Hispania kuna zaidi ya ndugu na dada 1,000 hivi wanaotumikia katika makutaniko 17 ya Kigalicia. Ndugu na dada hao wanahubiri habari njema kwa bidii.

Kikokola

Julai 11, 2025, Ndugu Marcelo Santos, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Msumbiji, alitangaza kutolewa kwa Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kikokola. Pia, alitangaza kutolewa kwa vitabu vifuatavyo: Marko, Luka, na Yohana katika lugha hiyo. Vitabu hivyo vilitolewa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa kwenye Jumba la Kusanyiko la Liciro katika wilaya ya Milange. Watu 1,445 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja wao alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo. Isitoshe, vitabu vyote vinne vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Hivi ni vitabu vya kwanza vya Biblia kutafsiriwa katika Kikokola. Ndugu na dada 2,300 hivi wanaozungumza Kikokola nchini Msumbiji wanafurahi kupata vitabu vyote vinne vya masimulizi ya Injili katika lugha yao.

Kimakua

Julai 11, 2025, Ndugu Castro Salvado, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Msumbiji, alitangaza kutolewa kwa toleo zima la Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika Kimakua. Tangazo hilo lilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Nampula. Watu 2,005 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana, na wengine 2,670 waliunganishwa kupitia video mtandaoni kutoka makusanyiko mengine matatu tofauti nchini Msumbiji. Kila mmoja aliyehudhuria makusanyiko hayo manne alipata nakala iliyochapishwa ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Biblia hiyo ilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa katika mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Isitoshe, rekodi za sauti za Biblia hiyo zilipatikana pia.

Watu milioni sita hivi wanazungumza Kimakua katika maeneo ya Kaskazini mwa Msumbiji. Kimakua ndiyo lugha inayozungumzwa na watu wengi katika maeneo hayo. Ndugu na dada zetu 2,600 hivi wanaotumikia katika makutaniko 60 ya Kimakua wana hamu kubwa ya kuitumia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika huduma, kwa ajili ya funzo la kibinafsi, na kwenye mikutano ya kutaniko.

Kiromani (cha Mashariki mwa Slovakia)

Julai 11, 2025, Ndugu Roman Roch, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Cheki na Slovakia, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiromani (cha Mashariki mwa Slovakia). Tangazo hilo lilitolewa katika Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Kosice, Slovakia. Watu 6,779 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana, na wengine 1,124 waliunganishwa kupitia video mtandaoni. Toleo hilo lilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Toleo lililochapishwa litapatikana baadaye mwaka huu.

Inakadiriwa kwamba watu 200,000 wanazungumza Kiromani (cha Mashariki mwa Slovakia) ulimwenguni pote, kutia ndani ndugu na dada zetu, zaidi ya 1,000. Isitoshe, katika eneo la ofisi ya tawi ya Cheki na Slovakia, kuna makutaniko kumi ya Kiromani (cha Mashariki mwa Slovakia) na kikundi kimoja. Pia, kuna makutaniko na vikundi kadhaa nchini Ujerumani na Uingereza vinavyozungumza lugha hiyo.

Kilendu

Julai 18, 2025, Ndugu Patrik Weiss, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa), alitangaza kutolewa kwa Biblia—Habari Njema Kulingana na Yesu katika Kilendu. Alitangaza pia kutolewa kwa vitabu vifuatavyo vya Biblia: Marko, Luka, Yohana, Waroma, na Wafilipi katika lugha hiyo. Tangazo hilo lilitolewa katika kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa kwenye Jumba la Kusanyiko la ITU Bunia Lumumba Yambi-Yaya katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Watu 477 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia—Habari Njema Kulingana na Mathayo. Isitoshe, vitabu hivyo vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Kuna watu milioni moja hivi wanaozungumza Kilendu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na katika sehemu mbalimbali za nchi ya Uganda. Leo, kuna zaidi ya ndugu na dada 560 wanaotumikia katika makutaniko 11 ya Kilendu kotekote katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na katika nchi ya Uganda.

Kinsenga (cha Zambia)

Julai 18, 2025, Ndugu John Musuba, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Zambia, alitangaza kutolewa kwa Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kinsenga (cha Zambia). Tangazo hilo lilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa huko Petauke, Zambia. Watu 2,165 walihudhuria kusanyiko hilo. Wale waliohudhuria walipata nakala zilizochapishwa za Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo. Toleo hilo lilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Kuna zaidi ya watu 405,000 wanaozungumza Kinsenga (cha Zambia). Leo, karibu ndugu na dada 11,000 wanatumikia katika makutaniko 145 ya Kinsenga (cha Zambia) nchini Zambia.

Kibasque

Julai 25, 2025, Ndugu Óscar Martínez, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Hispania, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kibasque. Tangazo hilo lilitolewa katika siku ya kwanza ya Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Donostia-San Sebastián. Watu 302 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana na wengine 49 waliunganishwa kupitia video mtandaoni. Wale waliohudhuria walipata nakala zilizochapishwa za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Pia, toleo hilo lilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye tovuti jw.org na kwenye programu ya JW Library.

Leo, Kibasque kinazungumzwa na zaidi ya watu milioni moja nchini Hispania. Ndugu na dada 250 wanatumikia katika makutaniko matano kotekote katika eneo la Kibasque.

Kimam

Julai 25, 2025, Ndugu Armando Ochoa, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Amerika ya Kati, alitangaza kutolewa kwa Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kimam. Alitangaza pia kutolewa kwa vitabu vifuatavyo: Marko, Luka, Filemoni, na Yuda katika lugha hiyo. Vitabu hivyo vitano vya Biblia, vilitolewa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Quetzaltenango, Guatemala. Watu 513 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana na wengine 80 waliunganishwa kupitia video mtandaoni. Kila mmoja wao alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo. Vitabu vyote vitano vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa katika mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Isitoshe, rekodi za sauti za vitabu hivyo vitano zilipatikana pia.

Inakadiriwa kwamba kuna zaidi ya watu 840,000 wanaoishi nchini Guatemala, Mexico, na Marekani wanaozungumza Kimam. Leo, ndugu na dada zetu 500 wanatumikia katika makutaniko 18 na kikundi kimoja cha lugha ya Kimam kwenye eneo la ofisi ya tawi ya Amerika ya Kati.

Kimanyawa

Julai 25, 2025, Ndugu Wayne Wridgway, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Msumbiji, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kimanyawa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” jijini Mocuba. Watu 781 walihudhuria kusanyiko hilo ana kwa ana na wengine 763 waliunganishwa kupitia video mtandaoni. Kila mmoja alipata nakala iliyochapishwa ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Toleo hilo lilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa katika mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu JW Library.

Hii ndiyo tafsiri ya kwanza iliyokamilika ya Maandiko ya Kigiriki kuwahi kutolewa katika Kimanyawa. Kuna watu 219,000 hivi wanaozungumza lugha hiyo kutia ndani ndugu na dada zetu 500 wanaotumikia katika makutaniko 13 ya lugha ya Kimanyawa nchini Msumbiji.

Kitaabwa

Julai 25, 2025, Ndugu Russel Ngoy, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa) alitangaza kutolewa kwa Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo katika Kitaabwa. Alitangaza pia kutolewa kwa vitabu vifuatavyo: Marko, Waroma, 1 Wakorintho, 2 Wakorintho, Wagalatia, Waefeso, Wafilipi, Wakolosai, 1 Wathesalonike na 2 Wathesalonike katika lugha hiyo. Tangazo hilo lilitolewa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa katika Jumba la Kusanyiko la Kasenga jijini Moba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Watu 3,958 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja alipata nakala iliyochapishwa ya Biblia―Habari Njema Kulingana na Mathayo. Pia, vitabu hivyo vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Isitoshe, rekodi za sauti za vitabu hivyo zilipatikana pia.

Kuna zaidi ya watu milioni 1.3 wanaozungumza Kitaabwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Leo, zaidi ya ndugu na dada zetu 1,700 wanatumikia katika makutaniko 35 ya Kitaabwa kotekote nchini.

Kiuruund

Julai 25, 2025, Ndugu Marcos Rozas, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa) alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiuruund. Alitangaza pia kutolewa kwa kitabu cha Biblia cha Wimbo wa Sulemani katika lugha hiyo. Tangazo hilo lilitolewa kwenye Kusanyiko la Eneo la 2025 la “Ibada Safi” lililofanywa jijini Musumba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Watu 1,769 walihudhuria kusanyiko hilo. Kila mmoja alipata nakala iliyochapishwa ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Vitabu hivyo vilikuwa tayari kwa ajili ya kupakuliwa kwenye mfumo wa kielektroni kwenye tovuti ya jw.org na kwenye programu ya JW Library. Isitoshe, rekodi za sauti za vitabu hivyo zilipatikana pia.

Kuna watu 153,000 hivi wanaozungumza lugha ya Kiuruund ambao wanaishi katika Mkoa wa Lualaba katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Idadi hiyo inatia ndani ndugu na dada zetu 627 wanaotumikia katika vikundi na makutaniko 16 ya Kiuruund.